Kamanda wa polisi Mkoa wa Katavi Ali Makame Hamad akizungumnza na waandishi wa Habari wa mkoa wa Katavi ofisini kwake [PICHA na Paul Mathias]
Mwanakijiji wa
Kitongoji cha Ipota Kijiji cha Ikuba Wilaya ya Mlele
Mkoa wa Katavi Shija Ntumbili anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukamatwa na meno ya Tembo mawili .
Kamanda wa Polisi wa
Mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame amewaambia Wandishi wa Habari kuwa mtuhumiwa
huyo amekamatwa kufutia msako makali uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa
kushirikiana na Askari wa Tanapa .
Amesema kabla ya
mtuhumiwa huyo kukamatwa jeshi la polisi walikuwa wamepata taarifa juu ya
mtuhumiwa huyo kujihusisha na biashara haramu ya meno ya Tembo .
Baada ya kuwa wamepata
taarifa hizo ndipo jeshi la polisi kwa kushirikiana na Askari wa Tanapa
walianza kufanya msako mkali .
Kamanda Ali Hamad Makame ameeleza kuwa kufuatia msako huu ndipo walipoweza kufanikiwa
kumkamata mtuhumiwa akiwa ameyahifadhi meno hayo ya tembo mawili
akiwa ameyahifadhi ndani ya nyumba yake .
Amebainisha kuwa
taratibu zinaendelee za kwenye idara husika ili kuweza kujua mano hayo
mawili yanathamani ya kiasi gani .
Amesema mtuhumiwa bado anaendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi na anatarajiwa kufikishwa wakati wowote Mahakamani ili akajibu tuhuma zinazo mkabili.
kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com