Na Paul Mathias Mlele-Katavi
Jamii imeaswa kuendelea kutunza mazingira ikiwemo kupanda miti ikiwa nisehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi ambayo yanashuhudiwa kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini.
Jamii imeaswa kuendelea kutunza mazingira ikiwemo kupanda miti ikiwa nisehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia nchi ambayo yanashuhudiwa kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini.
Hayo
yamebainishwa na mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi Onesmo Buswelu
wakati akizindua kampeni ya upandaji wa miti iliyofanyika katika Shule ya
Msingi Utende Buswelu, amesema kuwa
kwakutambua umuhimu wa Kuhifadhi mazingira kila mwanajamii anaowajibu wa
kutunza Mazingira kwenye eneo analoishi.
Buswelu
amebainisha kuwa serikali haitafumbia macho wale wote wenye tabia ya kuharibu
mazingira kwa kukata miti hawatabaki salama kwani serikali ipo macho pamoja na
taasisi za uhifadhi ikiwemo wakala wa mistu Tanzania Tfs pamoja na wadau
wengine wa uhifadhi wa mazingira.
Amesema miti hiyo iliyopadwa shuleni hapo ipatayo 2196 ilidwe na kutuzwa na kusiwepo na aina yeyote ya kuharibiwa na Mifugo kwakuwa kazi iliyofanyika nikwa masilahi ya uhai wa uhifadhi wa mazingira pamoja na viumbe hai kwakuwa uwepo wa miti mingi ndiyo chanzo cha mvua za kutosha ambazo hunyesha na kuufanya binadamu kufanya kazi kama kilimo na kazi zingine.
Aidha katikahatua nyingine ameagiza kuazishwa utaratibu wa uoteshaji wa Vitaru vya Miti katika maeneo ya shule na ofisi zingine katika ngazi ya Kata ili zoezi hilo liwe endelevu kwa wanachi kupanda miti pasipo kusubiria msukumo wa mamlaka za serikali.
Amesema kila kiongozi anapaswa kuwa balozi wa kuhifadhi mazingira kwakuwa swala la mazingira ni suala matambuka kwa kuwa linamhusu kila mmoja kwenye jamii yetu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Soudy Mbogo akipanda mti katika shule ya Msingi Utende ikiwa nisehemu ya kampeni ya upandaji miti katika mkoa wa Katavi.[PICHA na Paul Mathais] |
Amesema
halmashauri hiyo imeanza kusambaza miti katika taasisi mbalimbali kwaajili ya
kupanda miti hiyo kwenye maeneo hayo, Irafay amesema kuwa lengo lililopagwa na
halamsahuri hiyo ni kupanda miti ipatayo milioni moja na lakitano na kuisimamia
na kuhakikisha inafanyiwa uangalizi wa hali ya juu ili kuwa sehemu ya kutunza
mazingira.
“kazi
zilizofanyika ni kusafirisha miti hiyo kutoka eneo la uzalishaji na kuisambaza
katika taasisi mbalimbali ndani ya halmashauri ya Wilaya ya Mlele lakini pia
tumesimamia upandaji wamiti pamoja na kutoa maelekezo katika upandaji huo
lakini tumetoa elimu juu ya umuhimu wa kupanda miti katika maeneo tofauti kama
sehemu za baiashara na kaya” amesema Irafay
Msumeno
ametoa Rai kwa wanachi kutoendelea kuharibu mazingira kwa kukata miti kwani
kufanya hivyo nikuhujumu Rasilimali za mazingira hali ambayo hupelekea ukosefu
wa mvua.
Kwa habari zaidi tembelea ukurasa Wetu wa
kataviclub.blogspot.com