Wamachinga katika mkoa wa Katavi wakiwa kwenye zoezi la kukabidhiwa hati ya kiwanja kwaajili ya ujenzi wa ofisi yao eneo la kashaulili Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi[PICHA na Paul Mathias] |
Wafanya biashara wadogo wadogo maalufu kama wamachinga katika mkoa wa Katavi wameishukuru serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kulitambua Kundi hilo Rasimi kama makundi mengine.
Wafanya biashara wadogo wadogo maalufu kama wamachinga katika mkoa wa Katavi wameishukuru serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kulitambua Kundi hilo Rasimi kama makundi mengine.
Wamebainisha hayo wakati wa Makabidhiano ya Hati ya Kiwanja kilichotolewa na uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Katavi kama sehemu ya Maagizo ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kundi hilo kutambuliwa rasimi na kuwezeshwa miundombinu yao ili waweze kufanya kazi zao bila tatizo lolote.
Jennifer Evalist Mfanya biashara mdogo Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi amesema kupatiwa kiwanja na serikali ni hatua nzuri kwakuwa wao ni sehemu ya kuchangia pato kwa serikali kwa kazi wanazozifanya za baiashara ndogo ndogo.
“leo tumekabidhiwa Hati ya kiwanja
kwaajili ya wamachinga kujenga ofisi yetu hii itatusaidia sisi Machinga
kwaajili ya kuendeleza Shughuli zetu napenda kuishukuru Serikali kwa
kutuwezesha wametuheshimisha tutajikwamua kiuchumi” amesema Jennifer
wamachinga Mkoa wa Katavi wakifurahia jambo wakiwa kwenye makabidhaino ya hati ya kiwanja kwaajili ya ujenzi wa wa ofisi yao.[PICHA na Paul Mathias]. |
Ameeleza kuwa imekuwa bahati kwa mkoa wa Katavi kwa kuwapatia eneo na kuahidi kufanya kazi kwa bidiii kwakuwa serikali inawatambua Rasimi sasa.
Nae Aliki Gabriel mmoja wa Machinga
akizungumnza baada ya makabidhiano ya hati hayo kufanyika kwa wamachinga
amesema anaushukuru uongozi wa mkoa kwa kuwapatia kiwanja kwa sasababu walikuwa
wanapata changamoto ya kufanyia baishara zao.
“kwanza kabisa nipende kushukuruuongozi uliotupatia kiwanja kwa sasababu ilikuwa changamoto nyingi tulikuwa tunaziupata kabla hatujawa na sehemu ya kujenga ofisi leo hii tumeweza kupewa kiwanja kikubwa kuweza kujenga ofisi za wamachachinga nashukuru sana”
Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ambae alikuwa Mgeni Rasimi katika makabidhiano hayo ya Hati ya kiwanja kwa wamachinga wa Mkoa wa Katavi amesema anaushukuru uongozi wa machinga taifa kwa kuwa na shirikisho litakalo saidia kutatua changamoto za wamachinga kwa kushirikiana na serikali.
“kutokana na umuhimu wenu wafanyabiashara
ndogo ndogo mnafahamu kabisa kuwa na nimashuhuda kwamba Mh Rais Dk Samia suluhu
Hassan tangu aliposhika madaraka amekuwa akifanya mambo mengi kuhusu nyie
kuhakikisha kuwa mnatengenezewa mazingira mazuri,wezeshi na rafiki kwaajili ya
kufanyia biashara zenu kwa ufanisi” amesema Mrindoko
Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akiwahutubia wamachinga kwenye hafla ya kuwakabidhi hati ya kiwanja kwaajili ya ujenzi wa ofisi ya wamachinga mkoa wa katavi.[PICHA na Paul Mathias] |
Aidha katika hatua mkuu huyo wa
mkoa amesema halmashari zilizopo katika mkoa wa Katavi ziendelee kutenga maeneo
ya wamachinga pamoja na kuyawekea miundombinu rafiki sambamba na kuanzisha
Madawati yatakayo ratibu maswala ya wamachinga kwenye ngazi ya halmashauri.
“na sisi kama mkoa tutasimamia
kuhakikisha halmashauri zinaendelea kutenga maeneo kwaajili ya wafanya
baisahara ndogondogo,pia halmashauri zote ziwe na Madawati maalumu kwaajili ya
kuratibu na kuhudumia shughuli mbalimbali na mashauriano na wafanya biashara
wadogo wadogo wamachinga” amebainisha mkuu huyo wa mkoa.
Mwenyekiti wa Shirikisho la umoja
wa Machinga Mkoa wa Katavi Marko Ernest amesema
anamshukuru Rais Dk Samia suluhu hassan kwa kuagiza wamachinga kupatiwa maeneo
kwaajili ya kujenga ofisi agizo hilo limetekelezwa katika mkoa wa Katavi.
Amesema hiki kilichofanyika kwao
nitendo mhimu sana kwa sababu watajenga
ofisi ya kisasa na kuwasaidia katika shughuli zao za kila siku kwakuwa watakuwa
na ofisi ya kudunu.
Awali akitoa taarifa ya kazi za
wamachinga katika mkoa wa Katavi Ana Shumbi amesema mkoa wa Katavi unajumla ya
wamachjinga 3860 ambao wamekuwa wakiwatembelea kwenye maeneo yao juu ya utatuzi
wa changamoto zao zinazo wakabili.
Ameatoa rai kwa wamachinga katika mkoa wa Katavi kuendelea kujiunga katika shirikisho ili serikali iwe na urahisi wa kuwasaidia pindi fursa mbalimbali zinazojitokeza serikalini kupitia kundi hilo
kwa habari zaidi endelea kutembelea ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com