Kituo cha Afya Karema alipolazwa winfrida Athanasi baada ya kunyofolewa masikio yake na Mtoto wake wa Kumzaa [Picha na Walter Mguluchuma] |
Tukio
hilo la kusikitisha na la kikatili limetokea hapo juzi majira ya saa tano
usiku chumbani kwa mama huyo alipokuwa amelala kitandani .
Afisa
Mtendaji wa Kata ya Ikola Mwela Mrugwa amesema mama huyo
amenyofolewa masiko yake mawili na mtoto wake wa kumzaa mwenyewe
aitwaye Michael Msapi (40).
Siku
hiyo ya tukio mtuhumiwa Michael Msapi alimvizia mama yake mzazi
wakati akiwa amelala usingizi chumbani mwake na ndipo
alipoingia ndani ya chumba hicho na kumnyofoa masikio yake yote mawili
kwa kutumia meno yake na kumsababishia mama huyo maumivu makali sana .
Baada ya
kuwa amefanya ukatili huu kwa mama yake mzazi mhumiwa huyo alitokomea baada ya
kuwa mama yake amepiga mayowe ya kuomba msaada .
Mwela
Mnugwa amesema baada ya majirani kusikia mayowe hayo walifika haraka
kwenye eneo hilo na kumchukua Winfrida na kumkimbiza haraka kwenye
kituo cha Afya cha Karema ambako hadi sasa anaendelea kupatiwa
matibabu .
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Ally Hamad Makame amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo limeripotiwa katika jeshi la Polisi.
Amesema chanzo cha tukio hili ni Imani za kishirikina mtoto wa mama huyo Michael Msapi kumtuhumu mama yake kumloga mtoto wake .
Msako
mkali unaendelea wa kumsaka mtuhumiwa huyo kwani ametoroka mara tuu baada ya
kufanya tukio hili la kikatili.
kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com