DC : JAMILA HATUTAKUBALI WATOTO KUBAKI NYUMBANI BADALA YA KWENDA SHULE

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiwa katika moja ya darasa shule ya Sekondary Mpanda day kwenye ziara yake ya kuangalia hali ya Kuripoti kwa wanafunzi wa Kidato cha kwanza Shuleni Hapo[ picha na Paul mathias]

Na Paul Mathias- Mpanda.

Wazazi na walezi katika wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameonywa kutokuwa sehemu ya kuwakwamisha wanafunzi wa Darasa la awali, Darasa la Kwanza na Kidato cha kwanza kuanza masomo yao kwa mwaka huu wa 2023.

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiwa katika shule ya msingi Azimio katika ziara yake yenye lengo la kuangalia hali ya kuripoti kwa wanafunzi baada ya muhula wa masomo kuanza January 9 mwaka huu[picha na paul mathias]

Wazazi na walezi katika wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameonywa kutokuwa sehemu ya kuwakwamisha wanafunzi wa Darasa la awali, Darasa la Kwanza na Kidato cha kwanza kuanza masomo yao kwa mwaka huu wa 2023.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph wakati alipofanya ziara ya kuangalia hali ya Kuripoti kwa wanafunzi katika shule ya Msingi Ilembo,Shule ya Msingi Azimio,Shule ya Msingi Majengo na Shule ya Sekondary Mpanda Day zilizopo halmashauri ya Mnispaa ya Mpanda.

Akiwa katika Shule ya Sekondary Mpanda Day Mkuu huyo wa Wilaya amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha kwaajili ya ujenzi wa vyumba vya Madarasa amabapo katika Manispaa ya Mpanda wameafanikiwa kujenga vyumba 51 huku halmashauri ya Nsimbo wakifanikiwa kujenga vyumba vya Madarasa 27 kwaajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka huu 2023, Madarasa hayo yakiwa yameghalimu kiasi cha shilingi  bilioni 1, na milioni 560.

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila yusuph akiwa katika shule ya sekondary Mpanda day wakati alipotembelea shuleni hapo ilikujilidhisha hali ya kuripoti kwa wanafunzi wa Kidato cha kwanza mwaka huu[ picha na paul mathias]

Jamila amesema “tumegundua bado kuna wanafunzi mpaka sasa hivi bado hawajalipoti kuanza Darasa la awali,Darasa la kwanza na Kidato cha kwanza nitumie nafasi hii kutoa wito kwa wazazi na walezi wa wilaya ya Mpanda kuhakikisha mtoto yeyote aliefaulu kulipoti kwenye shule aliyopangiwa’’

Amebainisha kuwa tayari wamesha waagiza viongozi kuanzia ngazi ya Mitaa,Vijiji, watendaji na Mdiwani kuhakikisha wanahamasisha wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule kwani hakuna kisingizio kingine kwasababu miundombinu ya Madarasa ipo kwaajili ya wanafunzi hao.

‘’ mzazi yeyote ambae atazembea kutimiza huo wajibu wake wa kuhakikisha mtoto anaenda Darasa la kwanza ama Darasa la awali na kidato cha kwanza hatutamuacha tutamshughulikia kwa mujibu kanuni na taratibu za nchi hii amenena Jamila’’

Katika hatua nyingine amesema wameluhusu watoto kulipoti shule na kuanza masomo hata kama mzazi hajakamilisha taratibu za sale kwa mtoto wake hivyo hakuna kisingizio cha mzazi kutompeleka mtoto shule.

Akisoma taarifa ya hali ya uripoti kwa wanafunzi katika shule ya secondary Mpanda day Mwalimu mkuu msaidizi Moliwe Sanga amesema mpaka sasa wavulana 98 wameripoti shuleni hapo huku wasichana wakiwa  122 na kufanya jumla ya waliolipoti kufikia 200.

Mwalimu mkuu Msaidizi wa Shule ya Sekondary Mpanda Day Moliwe Sanga akisoma taarifa ya kuripoti kwa wanafunzi kwa mkuu wa wilaya ya Mpanda jamila Yusuph [Picha na Paul mathias]
Sanga ameeleza kuwa jumla ya wanafunzi 106 hawajaripoti Wavulana 44 na wasichana 62 na kufanya jumla ya wasiolipoti kufikia 106.

Awali Akizungumnza mbele ya mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila yusuph ,Mwalimu Adelahida Thomas Mwalimu wa Elimu maalumu katika shule ya Msingi Azimio ameiomba jamii kuacha tabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu kwani nao wanahaki ya kupata elimu kama watoto wengine.

Akiwa katika shule ya Msingi azimo mkuu wa wilaya Jamila yusuph amepata fursa ya kuzungumnza na walimu pamoja na kutembelea miundombinu ya madarasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu na kujionea ujenzi wa Bweni la wanafunzi hao ambalo limekamilika katika hatua ya kuezekwa.

 

 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages