Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi Ali Makame Hamad akizungumnza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati alipokuwa anatoa taarifa ya Matukio mbalimbali katika mkoa wa Katavi. |
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linawashikilia watu sita kwa tuhuma za kumuua mwalimu wa Shule ya Msingi Ugalla Wilaya ya Mpanda na kisha kumtupia mtoni baada ya kumfumania akifanya mapenzi na mke wa mtuhumiwa mwenzao.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Sud Athuman , Sangalo Said , Mrisho Hamis ,Juma Kanyama Malim Anton na Taus Hamis wote wakazi wa Kijiji cha Ugalla Wilaya ya Mpanda .
Ameeleza kuwawatuhumiwa hao wote sita walikamatwa mnamo Januari 9 mwaka huu majira ya saa nane usiku huko katika eneo la Kijiji cha Ugalla .
Kamanda Ali Makame
ameeleza kuwa mnamo tarehe 28 mwezi wa 12 mwaka
jana huko katika mto Ugalla zilipokelewa taarifa kuwa kuna
mwili wa mtu umeonekana unaelea ndani ya maji ya mto ugalla ugalla
ambae hakuweza kufahamika kwa jinawala surabaada ya kuwa mwili huo umeharibika
vibaya .
Baada ya mwili huo kuwa umeopolewa
ndani ya maji uchunguzi ulifanyika wa kidaktari na ndipo ulipo unyesha
kuwa mwili huu ulikuwa na majeraha ya kupigwa na uliweza kutambuliwa kuwa
ni mwili wa mwalimu wa Shule ya Msingi Ugalla baada ya uchunguzi
huo wa daktari msako ulianza wa kuwabaini watu waliofanya mauaji hayo .
Kufatia msako huo mkali uliofanywa na Jeshi la polisi ndipo mnamo tarehe 9/1/2023 polisi walipo weza kufanikiwa kuwakamata
watuhumiwa hao wote sita .
Kamanda Makame amebainisha kuwa
katika uchunguzi wa awali umebaini kuwa marehemu kabla ya
kuuawa alifumaniwa na mke wa mtu ndipo watuhumiwa hao
waliamua kumpiga na kumtupia mtoni .
Watu humiwa wote
wanaendelea kushikiliwa na Polisi na mara baada ya upelelezi kuwa
umekamilika watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazo wakabili