WAKULIMA WA PAMBA KATAVI BODI YA PAMBA NI MKOMBOZI WETU.


Wakulima wa zao la Pamba katika kijiji cha Mpembe wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wakiwa katika Mafunzo elekezi yaliyotolewa na watalamu kutoka Bodi ya Pamba Mkoa wa Katavi kuhusu  Matumizi sahihi ya Vinyunyizi na viwatilifu[Picha na Paul Mathias]

Na Paul Mathias -Katavi.
Wakulima wa zao la Pamba Katika vijiji vya Mpembe na Kapanga vilivyopo kata ya Katuma Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wamesema wanatalajia ongezeko la uzalishaji wa zao hilo kwenye Msimu huu kwakuwa wanaendelea kutembelewa na wataalamu kutoka Bodi ya Pamba kwa na kupatiwa elimu wakati huu wa kupulizia viwatilifu kwenye Mashamba yao.

Wakulima wa zao la Pamba kijiji cha Mpembe wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi
wakiwa katika picha ya Pamoja baada ya kupatiwa vifaa nyunyizi kutoka bodi ya
 Pamba   wakiongozwa  na Ramadhani Dissa  Mratibu wa kilimo cha zao la Pamba Katavi katikati mwenye Tisheti Nyeupe pamoja na Joseph Nyese Mkaguzi wa pamba wilaya ya Tanganyika wa Kwanza kulia [ Picha na paul mathias.

Wakulima wa zao la Pamba Katika vijiji vya Mpembe na Kapanga vilivyopo kata ya Katuma Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wamesema wanatalajia ongezeko la uzalishaji wa zao hilo kwenye Msimu huu kwakuwa wanaendelea kutembelewa na wataalamu kutoka Bodi ya Pamba kwa na kupatiwa elimu wakati huu wa kupulizia viwatilifu kwenye Mashamba yao.

Wakulima hao wamebainisha hayo baada ya kupatiwa elimu kuhusu namna bora ya Kupulizia Vinyunyizi dawa kwenye mashamba yao kutoka kwa watalaamu wa bodi ya Pamba mkoa wa Katavi walipofika kwenye mashamba yao kwa lengo la kutoa elimu hiyo kwa wakulima.

Welema Ochola Mkulima wa Pamba katika Kijiji cha Mpembe amesema wanamatumaini makubwa baada ya kupatiwa Elimu na vifaa kwaajili ya kupulizia Mashamba yao viwatilifu kutakuwa na ongezeko la uzalishaji tofauti na msimu uliopita.

Ochola anasema”kabla ya kupata pembejeo hizi ambazo ni sumu kwa wadudu waharibifu,Pampu pamoja na viwatilifu vingine kweli tulikuwa tunapitia wakati mgumu sana pamba ilikuwa inashambuliwa na wadudu na kuharibika sana tunaishukuru Bodi ya Pamba na NGS mnunuzi wa zao hili kwa kutupatia elimu na vifaa hivi’’

Wakulima wa zao la Pamba katika kijiji cha Kapanga wakiwa kwenye hatua ya kupalilia Magugu Shambani walipotembelewa na watalamu wa Kilimo Kutoka Bodi ya Pamba mkoa wa Katavi.[Picha na Paul mathias]

Ameendelea kuomba Bodi ya Pamba kuendelea kuwatembelea zaidi ili kuwapatia elimu na wanaimani kwa elimu hiyo kutakuwa na tija ya ongezeko la kilo za uzalishaji kwenye kilimo chao cha zao la Pamba.

Kwa upande wake Mabula Lugendenga Mkulima wa zao la pamba katika kijiji hicho amesema atakenda kuyafanyia kazi maelekezo aliyopewa na wataalamu wa kilimo kwani anamatalajio ya uzalishaji mkubwa kwenye ekali kumi alizolima msimu huu.

 Mashauri Maduhu mkulima wa pamba katika jijiji cha Kapanga amebainisha kuwa kunatofauti kati ya msimu huu na msimu uliopita katika eneo la pembejeo kwa kuwafikia kwa muda hali ambayo inawafanya kwenda sambamba na msimu wa zao hilo.

‘’mwaka huu naona kuna unafuu kunamwitikio kwa watalamu kuja kutusaidia, nimelima ekali nane nashukuru NGS na watalamu wa bodi ya pamba kwa elimu hii itaninufaisha kwenye kilimo changu amesema Maduhu”

Ramadhani Dissa Mratibu wa kilimo cha zao la Pamba kutoka Bodi ya Pamba  mkoa wa Katavi ameeleza kuwa wamekuja kusaidiana kuhakikisha msimu huu pamba yote iliyolimwa inafikia hatua ya kuvunwa.

Dissa ‘’amesema Misimu iliyopita walikuwa wanaotesha Pamba lakini inapofika wakati wa kutengeneza Vitumba inasahambuliwa na wadudu na visumbufu vingine vya Pamba na tatizo kubwa lilikuwa kwenye unyunyiziaji na vinyunyizi’’

Amebanisha kuwa Bodi ya Pamba itahakikisha wakulima wote wanapata vinyunyizi na viwadudu vinavyotakiwa ili kukidhi matakwa ya serikali.

Wakulima wa zao la Pamba kijiji cha Kapanga wilaya ya Tanganyika Mkoa wa katavi wakiwa kwenye picha ya Pamoja na viongozi wa Bodi ya Pamba mkoa wa katavi walipowatembelea kutoa elimu ya matumizi sahihi ya Vinyunyizi na kutoa vifaa vya unyunyiziaji wa zao la pamba kwenye mashamba yao.

Mratibu huyo amesema mkoa wa Katavi umepewa lengo la kuzalisha tani Elfu 14 tofauti na msimu uliopita walipojiwekea lengo la kuzalisha Tani Elfu 7, hivyo  tunatoa elimu hii ili kuhakikisha kwamba hilo lengo linafikiwa kwa manufaa ya serikali nayawanachi wote wa mkoa wa Katavi.

Joseph Nyese mkaguzi wa Pamba wilaya ya Tanganyika amesema bodi ya Pamba kwa kushilikiana ya na Kampuni ya  NGS iliyopewa Ridhaa ya kusambaza pembe jeo kwa wakulima wa zao la Pamba anasema wakuja na mpango maalumu wa kuzunguka kutoa elimu ya matumizi sahihi ya viwatolifu na vinyunyizi.

Nyese amefafanua kuwa mpango huo unakuja baada yakuona wakulima wengi kulalamika dawa kutofanya kazi waligundua kuwa baadhi ya wakulima kutokuwa na elimu sahihi ya vinyunyizi hivyo ndio maana wameanza kutoa mafunzo hayo kwa wakulima wakati huu wa kunyunyizia viwatilifu kwewnye mashamba yao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages