WAKULIMA WA TUMBAKU KATAVI HATARINI KUSHUKA UZALISHAJI KWA KUKOSA MBOLEA

 

Moja ya shamba la Tumbaku mkoa wa Katavi ambapo wakulima wamelalamikia kukosekana kwa Mbolea aina ya CAN[ PICHA na Walter Mguluchuma]

Na  Walter Mguluchuma-Katavi

Wakulima wa Tumbaku  Mkoani Katavi   wamelalamika  kukosekana  kwa mbolea  ya kukuzia  aina ya CAN  wakihofia kupata hasara wameiomba Serikali irudishe utararibu wa zamani wa Makampuni yanayonunua tumbaku yaruhusiwe kusambaza mbolea yenyewe.

Muonekano wa shamaba la Tumbaku katika katika kijiji cha Mchaka mchaka wilaya ya Tanganyika likiwa limekosa mbolea aina ya CAN kwaajili ya kukuzia  [Picha na Walter Mguluchuma]

Wakulima wa Tumbaku  Mkoani Katavi   wamelalamika  kukosekana  kwa mbolea  ya kukuzia  aina ya Can  wakihofia kupata hasara wameiomba Serikali irudishe utararibu wa zamani wa Makampuni yanayonunua tumbaku yaruhusiwe kusambaza mbolea yenyewe.

Wakizungumza na  mwandishi wa Habari  hii kwa nyakato tofauti  wakulima hao  wamedai kuwa  huenda msimu huu wakapata hasara kubwa kutokana na kuvuna tumbaku isiyo na ubora .

Wamedai kuwa mbolea ya can huchanganywa  na mbolea ya NPK  kwa ajiri ya kukuzia tumbaku  lakini pamoja na   muda wa kumadia mbolea hiyo kuwa imefika muda mrefu sasa  lakini  bado hawaja ipata .

 Mwenyekiti wa Amcos  ya Utense  Helmani Katala  amesema toka walipo panda tumbaku yao mwezi Novemba mwaka jana hadi sasa bado hawaja ipata .

Ameeleza kitaalamu  mkulima  hutakiwa  kusamadia  mbolea ndani ya siku saba  hadi 14 baada ya kupanda  lakini ni Zaidi ya miezi miwili sasa mkulima haja samadia jambo ambalo ni hatari kubwa kwa mkulima kuweza kukosa mapato .

Mkulima wa AMCOS   Mpanda Kati  Nassor  Ramadhan ameiomba Serikali  iangalie  utaratibu  uliokuwepo awali  wa Kampuni  za ununuzi wa Tumbaku  kusambaza mbolea kwa wakulima .

Amebainisha siku hizi wanapata mbolea kupitia  chama kikuu  cha ushirika LATCU  tumbaku inakaribia kuvunwa  kwa hiyo hata leo mbolea hiyo ikiletwa  haina faida kwa  baadhi ya wakulima  amesema Ramadhan.

Kokosekana kwa mbolea hiyo kunawafanya wao  kuzalisha tumbaku ambayo itakuwa  haina uzito unao takiwa na kusababisha uzalishaji wao kuwa  mdogo na tumbaku isiyo na ubora .

Ameeleza wakulima wa tumbaku wamekuwa wakihimizwa  na kusisitizwa  kulima na kupanda kwa wakati  na sasa wamefanya hivyo hata hivyo  wapo hatarini kula hasara .

Kauli hii imeungwa mkono  na  Richald  Kasogera  wa Amcos ya Ilela  Wilayani Mlele  akisema  kuchelewa  kwa mbolea  kunasababisha ubora wa tumbaku .

Pia uzito nao hupungua  na kufanya mkulima  zalisha   chini ya  malengo  yake na kusababisha hasara kwa mkulima .

Nae Deus  Bathromeo  wa Igagala Wilaya ya Tanganyika  amesema  tumbaku  ikikuzwa na Npk peke yake  huwa na rangi  ambayo sio ya chunjwa inayotakiwa kuwa nayo .

 Hali hii ni tofauti  kwa  wakulima  wa Amcos  ya Majalila  amesema wao hawana tatizo hili .

Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika LATCU  Mkoa wa Katavi  Venance  Dorashazi  amemwambia mwandishi wa habari hizi  kuwa wanatarajia kuipata mbolea ya can wakati wowote  wiki hii.

Amesema wamewasiliana na muungano wao  wa vyama vikuu vya ushirika vya mikoa ambao wanao wamewasiliana na YARA  kwa hali hiyo tatizo hilo litatatuliwa  shida ilikuwa ni kutofika mbolea hii kwa mapema .

Amesema  Amcos za Mishamo  kuwa ndio zimeathilika Zaidi  kwa kuwa hata cani ikifika  haitakuwa na kazi yoyote kwa kuwa wameisha anza kuvuna tumbaku na kuvichoma .

Pia ameeleza kuwa hata kwenye Amcos za Mpanda Kati , Nsimbo  Ilele , Utense na Ilunde  endapo kama wiki hii itapita bila kuwa wamepata mbolea haita ikifika baada ya hapo haitakuwa na kazi tena .

Kwa habari zaidi Tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages