MADIWANI WA CHACHAMAA BIASHARA YA VYUMA CHAKAVU


Baadhi ya Madiwani wa Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani [Picha na Walter Mguluchuma]

Na Walter Mguluchuma- Mpanda

 Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamelalamikia kitendo cha watoto wadogo kuzaa mitaani na kufanya biashara ya kuuza vyuma chakavu kwa wafanya biashara wa kununua vyuma chakavu .

Wiliamu Mbogo Diwani wa Kata ya Majengo akichangia hoja katika kikao cha baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda[ Picha na Walter Mguluchuma]

 Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamelalamikia kitendo cha watoto wadogo kuzaa mitaani na kufanya biashara ya kuuza vyuma chakavu kwa wafanya biashara wa kununua vyuma chakavu .

Malalamiko hayo wameyatoa leo  Januari 30   wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda

Diwani wa Kata ya Majengo Wiliamu Mbogo ameeleza kuwa kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wadogo  kuzagaa kwenye Kata ya Majengo  na  huku wakiwa wamebeba vyuma chakavu .

Mbogo ameshauri kuwa ni vema wafanya biashara wa vyuma chakavu wanao nunua kwa watoto wadogo  wakaonywa kuacha kufanya biashara na watoto  wadogo  kwani wanasababisha watoto kuzurula  na kueneo kwa wizi .

Amebainisha kuwa  hivi majuzi  umefanyika wizi wa miundo mbinu ya vyuma vya meza na  viti vya chuma kwenye shule   za Msingi za Azimo na Majengo  ambavyo inasadikiwa  vyuma hivyo  huuzwa kwa wafanya biashara wa vyuma chakavu ,

Diwani Mbogo ameeleza kuwa ni vema pia  wafanya biashara wa vyuma chakavu wakakumbushwa  kutonunua chuma chochote kile cha  Taasisi ya Seikali  kwani kufanya hivyo ni kuihujumu Serikali

Diwani wa Viti Maalumu Amina Kamande amesema kuwa tatizo la watoto kufanya biashara ya vyuma chakavi ni kubwa .

Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidari Sumry amelieleza baraza hilo la Madiwani kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamira Yusuph  alisha waonya wafanya biashara wa vyuma chakavu kutofanya biashara hiyo na watoto wadogo .

Ambapo  amesisitiza mfanya biashara atakae kutwa anafanya biashara hiyo na watoto wadogo Dc Jamira alisema  hatasita kumfutia leseni yake ya biashara ameliambia baraza hilo la madiwani  Meya Sumry

 kwa habari zaidi tembelea ukurasa wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages