Msitahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry wakati akifunga kikao cha Baraza la madiwani [Picha na Walter Mgluchuma] |
Na Walter Mguluchuma –Mpanda
Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidari Sumry ameagiza kuanzia sasa Wenyeviti wote wa Mitaa kwenye Halmashauri hiyo kulipwa posho zao kwa wakati.
Madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani [Picha na Walter Mguluchuma]
Sumry ametowa amaagizo hayo wakati alipokuwa akifunga kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda .
Amesema
kuwa licha ya wenyeviti wa Mitaa kufanya kazi kubwa sana lakini wamekuwa
wakicheleweshewa kulipwa posho zao .
Amebaisha
kuwa Wenyeviti hao wamekuwa wakifanya
kazi saa 24 za kusimamia Amani na
kusuluhisha migogoro mbambali kwenye maeneo yao .
Hivyo
kama Manispaa ni vema wakatambua mchango
wa kazi wanazo fanya kwa kuwatia moyo
kwa kuwalipa posho zao kwa wakati kwani ni haki yao ya msingi .
Aidha Sumry amewaomba
wandishi wa Habari waendelee kuwa hamasisha wananchi ambao watoto wao
hawajaripoti shule waweze kulipoti .
"Kwani
kuanzia Tarehe moja februari msako mkali utafanyika kwa wazazi wote ambao
hawtoto wao hawajaripoti shule hivyo wasiilaumu Serikali pindi"amesema Haidary .
kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu
kataviclub.blogspot.com