Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi akiwa kwenye ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa Mkoa wa katavi alipotembelea ofisini kwake. |
Na Walter Mguluchuma,Katavi
Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt Serafini Patrice amemwomba Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini aweze kwenda kuwasemia Serikali juu ya changamoto inayoikabili Hospitali hiyo ya kutokuwa na gari hata moja la Hospital.
Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt Serafini Patrice amemwomba Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini aweze kwenda kuwasemia Serikali juu ya changamoto inayoikabili Hospitali hiyo ya kutokuwa na gari hata moja la Hospital.
Ameomba
pia akawasemee na kuhusu shida walionayo
na MSD ambao wanavitu vingi sana vya kuleta katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi lakini
lakini wanavichelewesha .
Ombi hilo
amelitowa wakati wakati alipokuwa akizungumza na Mbunge huyo ofisini
kwake mara baada ya kuwa amemaliza
kuwafariji wagonjwa walilazwa katika Hospitali na wale walikuwa
wakitibiwa ambapo aliwafariji kwa kuwapatia vitu mbalimbali vikiwepo pampasi za
watoto na watu wazima sabuni na Juice.
Amesema Hospitali hiyo haina gari hata moja la ofisi
wanatumia gari zao binafsi ndogo kwani
Hospitali hiyo haijawahi kuwa na gar la ofisi
waliazimwa na gari moja na Wizara ambalo nalo ni mbovu ambalo limeharibikia Dodoma.
Dkt
Patrice amefafanua kuwa gari hilo
ambalo waliazimwa na Wizara
limeharibika huko huko Dodoma wakati
lilipokuwa ilimepelekwa kufanyiwa
matengenezo huko Dodoma .
Amesema wanashida na Bohari Kuu ya dawa (MSD) hivyo wanamuomba
Mbunge Kapufi aende akawasemee kwani
wanavitu vingi vya kuleta huku lakini
wanachelewesha .
Amebainisha
kuwa vifaa vya thamani ya nusu ya bilioni 5.9 ambavyo havija fika kwa ajiri ya
Hospitali Mpya lakini havija fika bado na vilitakiwa view vimefika toka mwezi
Desemba mwaka jana .
Mganga huyo amesema kuwa timu yake wamejipanga
kutowa huduma za kipekee na bora kwa
wateja wake na ameishukuru Serikali kwa
kuwaletea madakta nane wapya kwani waliokuwepo walikuwa saba .
Mbunge Kapufi
amesema Serikali imekuwa sikivu kwa kuendelea kutatua changamoto kwa
kuendelea kuleta wataalamu wa afya kwenye Hospitali kadri inavyowezekana ili kuepusha mtumishi
mmoja kihudumia watu wengi .
Mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Sebastiani kapufi akitembelea Wodi ya wagojwa na kuwapa pole siku ya Mwaka mpya 2023 |
Kunapo
kuwepo na vifaa tiba hata kazi ya Daktari inakuwa
rahisi hivyo watumishi wa afya wasichoke
kufanya kazi pindi inapokuwa kuna uchache wa vifaa.