WAHIMIZWA UADILIFU KWENYE UJENZI WA MIRADI

 

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi akiwa katika ziara ya kukagua Miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Mfuko wa Jimbo
Na Paul Mthias-Mpanda

Watalamu wa katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wameaswa kuzisimamia fedha za mfuko wa Jimbo kwa uadilifu ili zilete matokeo makubwa kwa wananchi kupitia Miradi ya maendeleo.

Wajumbe wa kamati ya mfuko wa jimbo la Mpanda Mjini wakiwa na Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo

Watalamu wa katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wameaswa kuzisimamia fedha za mfuko wa Jimbo kwa uadilifu ili zilete matokeo makubwa kwa wananchi kupitia Miradi ya maendeleo

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini Sebastian Kapufi wakati akiwa katika ziara ya kutembelea na Kukagua  Miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mfuko wa Jimbo 2021/2022 ili kulahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

Kapufia amesema kuwa kazi kubwa ya mfuko wa Jimbo ni Kuchochea na kusukuma maendeleo ya miradi mbalimbali kwa wananchi hivyo watalaamu wanaowajibu wa kufatilia na kufahamu mienendo ya Fedha hizo kwenye miradi katika maeneo yao kwa kina amesema kapufi

Ameeleza kuwa amelidhiswa na miradi hiyo licha ya baadhi ya miradi kuonekana kusuasua licha ya fedha hizo kutolewa na kuwaomba watendaji wa serikali kuzitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa kulingana na uhitaji wa maeneo husika

Katika hatua nyingine ameeleza kulidhishwa na majitolea ya wananchi katika miradi hiyo kwakuwa inaleta muunganiko mzuri kiutendaji baina yao na serikali hivyo miradi hiyo pindi inapokamilika kuwa sehemu ya umiliki wa wanachi wenyewe.

Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini akiingia katika moja ya mradi unaotekelezwa na Mfuko wa jimbo wakati wa kutembelea na kukagua miradi hiyo.

Paschal kadala mfanya biashara mdogo katika Soko la Kawalyowa amesema wamenufaika na mfuko wa Jimbo kwa kiasi kikubwa baada ya Mbunge wao kuwasaidia fedha kwaajili ya ujenzi wa soko la choo sokoni hapo.

Kadala amewaomba wafanyabiashara hao kuitunza Miundombinu hiyo ili iwezekudumu kwa muda Mrefu kwa munufaa ya sasa na baadae.

Kwa upande wake Maria Jonh mfanyabiashara wa Samaki katika siko la Kawalyowa amemshukuru Mbunge huyo kwa kuahidi kupaua eneo la soko hilo kwa Shilingi Milioni 10 ili waweze kufanya baishara zao katika mazingira Mazuri ya kiangazi na masika.

Katika ziara hiyo Kamati ya Mfuko wa jimbo ikiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi wameweza kutetembelea miradi  Kumi  kati ya kuminamoja inayochochewa na Mfuko huo wa jimbo yenye Samani ya Shilingi Milioni 41,000,000

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages