''UWT KATAVI NYIE NDIO MHIMILI WA CHAMA''

 

Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi CCM kutoka Mkoa wa Katavi akiwahutubia wanawake wa Jumuiya hiyo ya UWT Mkoa wa Katavi[Picha na Alex Ngereza]
Na Paul mathias- Katavi

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Gilbert Sampa amewataka Umoja wa jumuiya ya wanake ya chama cha Mapinduzi UWT Mkoa wa Katavi kutumia fursa ya kuwekeza miradi ambayo itakuwa na tija kwenye umoja wao.

Baadhi ya wanawake wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Katavi wakifurahia jambo baada ya kumalizika
kwa Shughuli walizozifanya za kupanda Miti kwenye ofisi za chama hicho kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 46 tangu kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi CCM[ Picha na Alex Ngereza]  
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Gilbert Sampa amewataka Umoja wa jumuiya ya wanake ya chama cha Mapinduzi UWT Mkoa wa Katavi kutumia fursa ya kuwekeza miradi ambayo itakuwa na tija kwenye umoja wao.

Akizungumza katika Sherehe ya miaka 46 ya kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi CCM Sampa amesema lazima Jumuiya hizo Kujikita katika miradi ya uchumi.

‘’Nyie kama UWT mnao uwezo wa kuanzisha vitega uchumi vitakavyo wasaidia kuiendesha jumuiya kwa kujikwamua kiuchumi kama chama chetu kinavyo sisitiza kubuni Miradi kwenye Jumuiya za chama chetu”amesema sampa.

Katibu wa itikadi na Uenezi wa chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mpanda Elias Mwanisawa akitoa neno kwa wanawake wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Katavi.[PICHA na Alex Ngereza]
Katika hatua nyingine amewaomba wanachama wa Jumuiya hiyo kushikamana na kufanya kazi kwa bidii ili kuifanya jumuiya hiyo kuendelea kuwa mhimili ndani ya chama cha Mapinduzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi Fotunata Kabeja ameshiriki katika zoezi la upandaji miti katika ofisi za chama hicho wilaya ya Mpanda pamoja na kuwatembelea wagojwa katika kituo cha afya Town Clinic.

Katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mpanda Elias Mwanisawa akitoa neno katika hafla hiyo amesema kila mwanachama anawajibu wa kuyatangaza kwa kifua mbele yale yote yaliyotekelezwa na Serikali ya Dk Samia Suluhu Hassan kwa vitendo.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake ya chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Fotunata Kabeja akipanda Mti kwenye eneo las ofisi ya Chama hicho wilaya ikiwa ni sehemu ya sherehe za kuzaliwa kwa chama cha Mapinduzi[ Picha na Alex Ngereza]
“ndugu viongozi tusikubari mtu atakayeonekana kubeza juhudi ambazo Rais wetu amezifanya kwa nguvu kubwa”amesema mwenezi huyo.

 Mwenezi huyo amesema chama cha Mapinduzi kitaendelea kuwatumukia wanachi na wanachama wa chama hicho bila kujali Rangi,na itikadi zao kwakuwa chama hicho ndicho kilicho pewa ridhaa ya kuwaongoza kupitia serikali ya chama cha Mapinduzi

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages