MWENYEKITI MSTAAFU BEDA AUNGURUMA " SIKUJIITA DAKTARI".

 

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi,Beda Katani akizungumza ya kina na chombo hiki hivi karibuni- (Picha na Paul Mathias)

Na George Mwigulu,Katavi.

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi,Beda Katani anajivunia mafanikio ya zaidi ya miaka 20 ya kukitumikia chama hicho kwa nyadhifa mbalimbali licha ya kutokuweza kuonekana kwenye duru nyingine ya uchanguzi wa ndani uliofanyika hivi karibuni.

Mwenekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi,Beda Katani akisisitiza jambo wakati wa mahojiano maalumu- (Picha na Paul Mathias)

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi,Beda Katani anajivunia mafanikio ya zaidi ya miaka 20 ya kukitumikia chama hicho kwa nyadhifa mbalimbali licha ya kutokuweza kuonekana kwenye duru nyingine ya uchanguzi wa ndani uliofanyika hivi karibuni.

Akizungumza na chombo hiki kwenye mahojiano maalumu katika viunga vya Garden Park Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi anasema mafanikio yake sio ya kutiliwa shaka ndani ya CCM,Serikalini nakwa wananchi wa hali chini.

Beda ameweka wazi juhudi zake za kuwaunganisha wanachama na kuiamini serikali yao iliyoundwa na CCM kuwa ndio kimbilio na mwarobani wa matatizo yao.

Anabainisha kuwa wakati anaingia ndani ya uongozi ndani ya chama hicho hali haikuwa shwari kutokana na baadhi ya maeneo kuwa ngome ya upinzani hali hiyo ilimpa hamasa ya kufanya kazi kwa bidii ya kisiasa ili kukomboa maeneo hayo na kuwa chini ya CCM kwa mfumo halali wa kidemokrasia unaotambuliwa na Katiba ya nchi “ Nilitumia weledi na siasa safi kushawishi umma kukiamini chama Tawala”amebainisha.

Katika kutatua matatizo ya wananchi alifungua milango muda wowote akiamini kwamba suluhu ya matatizo ya wananchi yanakabiliwa kwa kuyatatua kwa vitendo.

CCM imekuwa dira na mwongozo kwa watendaji wa serikali kwa kuhakikisha ilani ya chama inatekelezwa na wakati mwingi ilimbidi kuwa mkali kukemea ubadirifu wa fedha za umma na uzembe kwa masirahi ya wananchi bila kujali itikadi zao.

“…nakumbuka nikiwa na Kamati ya Siasa ya Mkoa nilitembelea Kata ya Mwamkuru na kubaini msingi moja ya majengo ulikuwa umejengwa chini ya kiwango na nilitambua hivyo baada ya kuomba jembe na kutindua na nilijionea kiwango kidogo zaidi cha cementi kilichokuwa kimetumika kujengea” Amesema Beda.

Amesema Msitaafu huyo “Baada ya kitendo hicho wataalamu walikuja na kubaini kile nilichokiona mimi,na ndipo jina la Mhadisi nilipolipata kwa kuwa nao walijiridhisha kwa kubaini mapungufu hayohayo ambayo nami niliyabaini kwa macho na hisia zangu”.

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi,Beda Katani (wa pili kulia) wakati akiwa Mwenyekiti wa Chama hicho pale alipompokea Makamo Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Abdurahaman Kinana  mnamo mwenzi Julai mwaka jana - (Picha na Maktaba ya KatavI Press Club)

Vilevile ameeleza kuwa uhodari wake wa kutafuta ufumbuzi kwenye masuala kadha wa kadha magumu ya wananchi kwa kuamini kuwa akitatua matatizo ya wananchi ndiyo salama ya Serikali na CCM.

“Kazi za ufumbuzi wa matatizo zilinifanya niitwe Daktari” ameweka wazi hivyo.

Kuhusu uwajibikaji kwa watendaji  wa serikali ndani ya uongozi wake inatajwa kuwa alikuwa mkali.

 “…labda watu wananitafsri ukali wangu ulikuwa katika sura ya kiutendaji kwa kuamini kuwa kazi ya chama ni kuisimamia serikali”amesema hayo huku akieleza kuwa uongozi wake ulikiunganisha Chama na Serikali na hapakuwa na uadui wowote dhidi ya watumishi wa serikali na chama.

“…kunakosa gani la kumpigia simu kiongozi Mhandisi, au Meneja yeyote wa Taasisi ya umma kwa lengo la kufahamu namna wanavyotatua shida za wanachi kupitia malalamiko ninayoyapata kutoka kwa wananchi?.“ alihoji Beda”

Aidha anaamini ufumbuzi wa mataizo ya wananchi utaendelea kufanyika ndani ya uongozi mpya kwa kuwa CCM inawanachama imara na wenyewe uwenzo mkubwa wa kufanya kazi kwa masirahi mapana ya Chama na Taifa kwa ujumka huku akisema kuwa Chama amekiacha kikiwa na nguvu na kuaminiwa na wananchi.

Mwendelezo wa Makala hii itakuwa wiki ijayo ambapo Mh Mwenyekiti Mstaafu CCM Mkoa wa Katavi,Beda Katani ataelezea ni namna gani alivyopokea utenguzi wa zuio la mikutano ya hadhara na Mh Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Tufuate kwenye kusarasa zetu Twitter/Instagram @katavipc na Facebook Katavi Press Club.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages