WAZIRI NAPE AWASIFU WANAHABARI KATAVI "TUTAPATA WABOBEZI WAKUTOSHA"


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akiwa mkoani Katavi kwa ziara ya siku mbili - (Picha na Paul Mathias)

Na George Mwigulu, Katavi

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amewapongeza wanahabari wa Mkoa wa Katavi kwa kuendelea kuandika habari zinazoutangaza mkoa wa huo kwenye mambo mbalimbali.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akisalimiana na viongozi mbalimbali wa kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa wa Katavi.
(Picha na Paul Mathias)
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amewapongeza wanahabari wa Mkoa wa Katavi kwa kuendelea kuandika habari zinazoutangaza mkoa wa huo kwenye mambo mbalimbali.

Amesema hayo leo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwamvua Mrindoko baada ya  kusomewa taarifa ya mkoa akiwa kwenye ziara ya siku mbili ya kikazi mkoani hapa.

Nape ameeleza kuwa amekuwa akizisikia habari za Mkoa wa Katavi kupitia vyombo  vya habari vikielezea masuala  mbalimbali.

“niwapongeze wanahabari wa Katavi tunazisikia habari za Katavi…RAS anasema hawapo wabobezi lakini wabobezi wanatengezwa taratibu na mimi naamini katika kazi hiyo hiyo mnayoifanya basi  tutapata wabobezi wa kutosha” Amesema Nape.

Aidha amesisitiza kuwa wizara hiyo itaendelea kuhamasisha watu kuja kuwekeza wenye sekta ya mawasiliano na habari kwa kuwa mkoa wa Katavi unakua kwa kasi na kuwa na mabadiliko makubwa.

Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi (waliosimama) wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi- (Picha na  Paul Mathias)

Vilevile kwa upande waandishi wa habari wa Mkoa wa Katavi wakisema kwa masharti ya kutokutajwa jina lake ameeleza kuwa viongozi wa Mkoa wa huo watambue umuhimu wa waandishi wa habari kwa kuwa kiungo cha utendaji kazi  baina yao na wananchi wanaowatumikia.

Ameeleza kuwa kitendo cha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye kuwapongeza waanahabari hadhari mbele ya viongozi mbalimbali wa mkoa ni ishara njema ya kuacha somo ambalo kama litafanyiwa kazi litaweza kukuza tanisia ya habari.

Alex Ngereza Mwandishi wa habari wa Radio Free Africa na Start Tv wa Mkoa wa Katavi ameishukuru serikali kupitia waziri Nape kwa kuona mchango wa waandishi wa habari akishauri kuwa kama wizara husika imeona juhudi za kuhabarisha umma zinazofanywa na kundi hilo.

Amefafanua kila kuna haja ya serikali ya mkoa wa Katavi kuangalia namna bora ya kuweka mazingira wezeshi ya kuwainua kiuchumi kupitia kazi wanazozifanya.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages