RC MRINDOKO ATOA SIKU SABA KWA SUMA JKT.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindo (katikati) akiwa kwenye ukaguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo ambapo ameongozana na Katibu Tawala,Abas Hassan Rugwa (kushoto) na Mganga Mfadhi wa Hospitali hiyo Dkt Serafini Patrice (Picha na George Mwigulu) 

Paul Mathias na George Mwigulu,Katavi.

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko ametoa siku saba kwa Mkandarasi Suma JKT anaetekeleza Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa  Mkoa wa Katavi kuhakisha anasambaza umeme kwenye jengo la Hospital ya Rufaa iliyopo eneo la kazima Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi,Abas Hassan Rugwa (Kulia) akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa huo,Mwanamvua Mrindoko wakati wakitembelea na kukagua Hosptali ya Rufaa ya Mkoani hapa (Picha na George Mwigulu)

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ametoa siku saba kwa Mkandarasi Suma JKT anaetekeleza Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa  mkoa wa katavi kuhakisha anasambaza umeme kwenye jengo la Hospital  iliyopo eneo la kazima Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Agizo hilo amelitoa wakati akipokea vifaa vitakavyopotumika kusambaza umeme kwenye jingo hilo alipotembelea hospitali hapo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Waziri mkuu Kassimu Majaliwa alipofanya Ziara ya Kikazi katika mkoa wa Katavi mwaka jana na kuagiza  umeme kusambazawa kwenye Jengo hilo la hospitali.

Mwanamvua Mrindoko (katikati),Mkuu wa Mkoa wa Katavi akitoa maelezo juu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo ambapo ametoa maelekezo kwa SUMA JKT kuhakikisha miundoimbinu ya umeme inatengenzwa kwa wakati muafaka.
Mganga Mfawidhi wa Mkoa wa Katavi,Dkt Sarafini Patrice akitoa maelezo kwa Mkuu wa  Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko juu ya mwenendo wa upokeaji wa vifaa tiba hospitalini hapo (Picha na George Mwigulu)

Akiwa Hospitalini hapo Mwanamvua amesema tayari Vifaa kwaajili ya usambazaji wa umeme vimeshafika kwaajili ya kutekeleza agizo hilo la Waziri Mkuu pamoja na kwamba tayari kuna kuna baadhi ya huduma zimeanza kutolewa hospitalini Hapo.

Amesema “lakini nimwagize Mkandarasi Suma JKT tumempa siku Saba kuhakikisha kazi hii ya kuingiza umeme huu ndani inakamilikai na ifikakapo Tarehe 15/1/2023 hii kazi iwe imekamilika na huduma hapa zitolewe”

Amemwelekeza Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi Serafini Patrce kuhakisha kuwa vifaa tiba vyote vilivyoletwa na serikali kukaka sehemu husika tayari kwa kuanza kufanya kazi ya kuhudumia wananchi baada ya kumalizika kwa kazi ya kusambaza umeme katika jenngo hilo la Hospitali ya Rufaa Mkoa wa katavi.

Aidha katika hatua amewaomba wanachi wa mkoa wa katavi kujisikia fahari kwa serikali yao ya awamu ya Sita ya Dk Samia Suluhu Hassani kwa uwekezaji katika sekta ya afya hasa kwa ujenzi wa hospitali ya rufaa mkoa wa katavi ili wananchi wapate huduma mbalimbali bila kufuata huduma hizo mikoa mingine.

Ni moja ya majengo yanayopatikana katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi ambapo imeigharimu serikali kiasi cha fedha zaidi ya Bilioni 12  kwenye ujenzi wake.
(Picha Na George Mwigulu)

Ni moja ya majengo yanayopatikana katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi ambapo imeigharimu serikali kiasi cha fedha zaidi ya Bilioni 12  kwenye ujenzi wake.
(Picha na George Mwigulu)

Ni sehemu ya Nyaya zitakazo tumika kuuganisha umeme katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi ambazo zimewasili leo Tarehe 07,January ,2023.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa katavi Dkt Serafini Patrice amesema tayari vifaa mbalimbali ikiwemo vitanda vimeanza kuletwa ikiwanisehemu ya mpango wa serikali kuipatia hospitali vifaa kwaajili ya kuanza kazi ya kuhudumia wananchi.

Ameeleza kwa Mwezi huu wa kwanza wanatalajia kupokea vifaa vyenye samani ya shilingi bilioni Tano ingawa hadi sasa  wameshapokea vifaa mbalimbali vyenye samani ya shilingi Bilioni Moja kutoka Bohari ya Madawa [MSD] huku wakiendelea kusubilia vifaa mbalimbali kwaajili ya hospitali hiyo.

Mradi wa ujenzi wa hospitali ya rufaa mkoa wa Katavi kukamilika kwake na kuanza kutoa huduma ni faraja kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kuepuka adha ya kufata Matibabu Makubwa katika mikoa ya Mbeya mwanaza na Tabora.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages