NAPE: UTAPELI MTANDAONI HAUKUBALIKI


Waziri wa Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Nape Nauye [katikati mwenye Shati Jeupe] akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Halmashauri ya Mlele Mkoa katavi baada ya kuzindua Mnara wa TTCL katika eneo la Inyonga yalipo makao makuu ya halmashairi hiyo [Picha na Paul mathias]
Na Walter Mguluchuma-Katavi

Waziri wa Mawasiliano na Tekinojia ya Habari Nape Nauye amewataka Tanzania  kutumia vizuri  mawasiliano  kwa kuweza kujiajiri na wasitumie mawasiliano kwa kutapeli watu bali watumie kwa kujiletea maendeleo .

Mkurugenzi  Mkuu wa TTCL Peter Ulanga akitoa maelezo kwa Waziri wa Mawasiliano na Technolojia ya Habari Nape Nauye katika eneo ulipojengwa mnara wa TTCL
Inyonga halmshauri ya Mlele Mkoa wa Katavi[Picha na Paul mathias]

Waziri wa Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Nape Nauye amewataka wa Tanzania  kutumia vizuri  mawasiliano  kwa kuweza kujiajiri na wasitumie mawasiliano kwa kutapeli watu bali watumie kwa kujiletea maendeleo

Wito huu ameutowa Wilayani Mlele  Mkoani Katavi wakati alipokuwa akizindua  mnara wa mawasiliano  uliojengwa na TTCL kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano kwa wote.

Amesema  watanzania watumie uwepo wa mawasiliano kwa kujipatia ajira na kwa ajiri  ya maendeleo na wasitumie vibaya kwa kutapeli  kudanganya watu na kudanganya watoto wadogo wa kike wanafunzi .

Nape amebainisha kuwa  tutumie uwepo wa masiliano kwa vijana kuweza kujiajiri  na tusitumie kwa umbea tutumie kwa ajiri ya maendeleo ya kilimo na katika biashara mbambali zitakazo weza kutupatia fedha .

Amesema  miradi hiyo ya minara imejengwa kwa fedha za walipa kodi wananchi hivyo ni mali ya wananchi wenyewe hivyo  wailinde ,waitunze  waisimamie ni rahisi kuzani kwa kuwa imejengwa na TTCL na  mamlaka ya  mawasiliano na kudhani kuwa si mali ya wananchi , wao kazi yao kama Serikali ni kuiliendelea kuihudumia waitunze  hivyo  wananchi  wailinde.

Waziri wa Mawasiliano na Tekinolojia ya Habari Nape Nauye akitoa neno baada ya kuzindua mnara wa TTCL Katika halmashauri ya Mlele Mkoa wa Katavi [picha na paul mathias] 
Amewataka  waitumie  kwani  itakuwa ni kazi bure kujenga minara ya kisasa kwa gharama kubwa halafu watu wasiitumie  Serikali inajua simu  za kisasa gharama zake ni kubwa  hivyo  imeanza mazungumzo na watoa  huduma mbalimbali ya mitandao  waanzishe utaratibu kwa watu kupata simu za kisasa hata kwa mkopo na mazungumzo yanakwenda vizuri .

Mkurugenzi Mkuu waMfuko wa  Mawasiliano kwa wote Justina  Mashiba amesema  mamlaka hiyo  inatekeleza  shughuli zake kwa kuwa na miradi  Nchi nzima kwenye kila Wilaya ya na Mkoa .

Mashiba amebainisha kuwa hadi  sasa wameisha kushirikiana na watowa huduma mbambali wa mawasiliano  kama TTCL , Tigo   Voda com,Airtel na Makampuni mengine wameisha saini mikataba ya ujenzi wa minara  1242 ya mawasiliano kwa nchi nzima na kati ya minara hiyo minara 1087 imeisha kamilika .

Amesema  minara  ambayo iliyobakia  kujengwa ni  155 ambayo nayo ipo kwenye hatua mbambali  za ukamilishwaji na itakapokuwa imekamilika itakuwa  minara  1242 watakuwa wamewafikia Wanzania milioni 15.

Mkurugenzi  Mkuu wa TTCL Peter Ulanga  amesema  TTCL  inaendelea kuboresha mawasiliano  kwenye maeneo yote ambayo hayana mawasiliano yakiwepo maeneo ya mikoa ya pembezoni.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages