RC KATAVI: HAIWEZEKANI MBOLEA ZIWEPO HALAFU SITIKA ZIKOSEKANE.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akigagua Moja ya Ghala la kuhifadhia mbolea katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi- (Picha na George Mwigulu)

Walter Mguluchuma na Paul Mathias,Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ameyaagiza  makampuni yanayosambaza mbolea Mkoani Katavi Kuhakikisha Mbolea yote  ambayo imeletwa Mkoani Katavi  iwafikie wakulima haraka iwezekanavyo ili wakulima waendelee na shughuli za kusamadia Mazao yao Mashambani.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akipata maelezo ya zoezi la usambazaji wa mbolea kwa wakulima kutoka moja ya Makampuni ya usambazaji wa mbolea Mkoa wa Katavi- (Picha na George Mwigulu)

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ameyaagiza  makampuni yanayosambaza mbolea Mkoani Katavi Kuhakikisha Mbolea yote  ambayo imeletwa Mkoani Katavi  iwafikie wakulima haraka iwezekanavyo ili wakulima waendelee na shughuli za kusamadia Mazao yao Mashambani.

Maagizo hayo ameyatoa wakati alipotembelea na kukagua Maghala ya Mbolea yaliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi amesema makampuni yoye yanayoleta mbolea Mkoani Katavi wahakikishe  mbolea hiyo inawafikia wakulima kwa wakati na hato sita kuchukua Hatua kwa Makamuni yatakayo Saza Mbollea hiyo kwenye Maghala ya hayo ya kuhifadhia mbolea pasipo na sababu yoyote ya kutosambaza mbolea kwa wakulima.

Mrindokoa amesisitiza kuwa agizo hilo halina mjadala wala majadiliano agizo ni kutekelezwa kwa muda huo alioutowa wakulima wawe wamepata mbolea yao na kwenda nayo shambani kwa ajiri ya kwenda kutumia kwenye mazao yao waliolima shambani kwao .

Amesema kuwa msimu wa mvua Mkoa wa Katavi unawahi kuanza kuliko ilivyo kwenye mikoa mingine hivyo  Mkoa wa Katavi wanachokihitaji ni mbolea   kwani mvua zinaendelea kunyesha na mbolea kuendelea kukaa kwenye Maghala pasipo kuzisambaza kwa wakulima ni Kufanya Hujuma kwa wakulima nakwa  Serikali ya Dk Samia Suluhu Hassan.

Ameyaonya Makampuni yanayoleta  mbolea Mkoani Katavi  hawata yavumulia Makampuni yanayoleta visingizio kuwa wanashindwa kugawa mbolea  kwa kisingizio kuwa hawana sitika hali ambayo imekuwa ikisababisha uchelewashaji na kuwafanyawakulima kupanga foleni kubwa kwa muda mrefu kwa mawakala .

Muonekano wa mbolea zilizo hifadhiwa katika Ghala la kuhifadhi mbolea zilizoletwa na serikali kupitia ruzuku kwa wakulima- (Picha na George Mwigulu)

Mrindoko amesisitiza kuwa Onyo hilo sio kwa makampuni tu bali  hata kwa mawakala  au msambazaji wa mbolea amabao wamepata kazi hiyo ya usambazaji kuifanya kazi hiyo kwa mujibu wa makubaliano baiana yao na serikali.

Katibu Twala msaidizi sehemu  uchumi na uzalishaji  wa Mkoa wa Katavi Nehemia Jemes amesema Mkoa waKatavi  kwa msimu huu wa kilimo umepangakutumia tani  14,811  kati ya tani hizo tani 7,406 ni za mbolea za kupandia na tani 74,405 ni mbolea za kukuzia ambapo mkoa umepanga kuzalisha tani 1,160,000 za mazao mbalimbali ya chakula msimu huu,

James ameishukuru serikali kuweza kutoaya shilingi Bilioni 150 kama ruzuku kwa wakulima nchinzima kwani imekuwa mkombozi mkubwa sana kwa wakulima wa Mkoa wa Katavi ambapo hadi sasa tani 6,539 zimeisha   ingia shambani na kusamadia mazao ya wakulima.

Mkulima Hadson Kombe amesema wamekuwa wakipata changamoto ya uhaba wa mbolea ya kukuzia mazao huku mbolea nyingi iliyopo niyakupandia.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages