TAMISEMI KUSHUGHULIKIA TATIZO LA KIINGEREZA MASHULENI.


Mkurugenzi wa Uboreshaji Elimu kutoka TAMISEMI Vicent Kayombo akitoa maelezo mbalimbali kwa wadau walio hudhuria kikao kazi cha kuboresha elimu ya msingi na sekondary Katika mkoa wa Katavi.[Picha na Paul mathias]
Na  Walter Mguluchuma - Katavi
Wizara ya TAMISEMI  wamekusudia  kuandoa tatizo la wanafunzi wa Shule za Msingi  linalo wakabili la kutojua kusoma na kuandika na wanafunzi wanao maliza kidato cha nne kutojua kuzungumza lugha ya kingereza .

Washiriki mbalimbali wa kikao kazi cha kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondary kilichofanyika katika ukumbi wa  Mpanda Social hall Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi.[ Picha na Paul mathias] 

Wizara ya TAMISEMI  wamekusudia  kuandoa tatizo la wanafunzi wa Shule za Msingi  linalo wakabili la kutojua kusoma na kuandika na wanafunzi wanao maliza kidato cha nne kutojua kuzungumza lugha ya kingereza .

 Hayo yamesemwa na Mkurugenzi  wa usimamizi wa Elimu wa Tamisemi Vicenti Kayombo  wakati wakikaokazi cha uboreshaji wa Elimu ya Msingi na Sekondari  katika Mkoa wa Katavi kilichofanyika katika Ukumbi wa Madini wa   Manispaa ya Mpanda .

Amebainisha kuwa  kumekuwa na tatizo la wanafunzi wa  Shule za Msingi  kutojua kusoma nakuandika  hali ambayo imepelekea kuna Shule moja ya Msingi hapa nchini kukosa kuwa na darasa la tano kufuatia wanafunzi wote wa darasa la nne kufeli mtihani .

Amefafanua kuwa  hata kwenye Shule za Sekondari kumewepo na changamoto ya   baadhi ya wanafunzi wanao maliza elimu ya kidato cha nne kutojua kuongea lugha ya Kingereza .

Katibu Tawala mkoa wa Katavi Abbas Hassan Rugwa akiwahutubia wajumbe wa kikao kazi cha kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondary ambapo amsema mpaka sasa ni asilimia 25 ya wanafunzi walioripoti shuleni kuanza kidato cha kwanza.[Picha na Paul Mathias]
Kayombo amesema kuwa  TAMISEMI  wamekusudia  kuondoa  tatizo la  watoto kutojua kusoma  na kuandika  kwenye shule za Msingi na kwenye Sekondari kuzungumza Kingereza  wanaamini kuwa hilo lina wezekana .

Amesisitiza kuwa kuanzia sasa walimu wanao kuwa wanafundisha watoto wa darasa la kwanza na lapilli wawe ni wale wenye nguvu kuliko ilivyo sasa jukumu hilo wameachiwa walimu wazee  kwa kile kinachoelezwa wakacheze na watoto .

Pia walimu wanaofundisha  darasa la saba wawe wanashuka kufundisha hadi darasa la tatu kuliko ilivyo sasa wanafundisha  madarasa ya juu tuu.

Kuhusu elimu ya Sekondari  ameeleza kuwa kuna changamoto ya  wanafunzi mpaka wanamaliza kidato cha nne unakuta wanakuwa hawajuwi kuongea lugha ya Kingereza

 Kayombo amesema kuwa swala la kusisitiza wanafunzi wajuwe lugha ya kingereza  sio kwamba wanauwa lugha ya Kiswahili bali  wanatekeleza Sheria ya Elimu ya waka 2014.

Hivyo kuanzia sasa walimu wote wa Shule za Sekondari pamoja na wanafunzi wao  lazima wawasiliane kwa lugha ya kingereza .

Amesisitiza kuwa hata Diwani akifika shuleni kutembelea nae  apewe maelezo kwa lugha ya kingereza na Maafisa elimu Kata wanapokuwa wanakwenda kukagua ukaguzi wao wafanya mazungumzo kwa kutumia lugha ya kingereza tuu.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi amewataka walimu waeshimu maadili  kwani kufanya hivyo watakuwa wameimarisha elimu .

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Hassan Lugwa amesema kuwa hadi sasa kati ya wanafunzi 14.904 waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza ni wanafunzi asilimia 25 tuu ndio wameisha ripoti shuleni .

 Enndelea kutufatilia kwa habari zaidi kwenye ukurasa wetu wa .

kataviclub.blogspot.com

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages