RC MRINDOKO KUKOSA SARE ZA SHULE SIO KIKWAZO CHA KUTOSOMA.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko akisoma taarifa ya Mkoa wa Katavi kuhusu Maendeleo ya Elimu kwa Mkoa wa katavi wakati wa kikao kazi cha kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondary kwenye Mkoa wa Katavi. Picha na Paul Mathias]
Na walter Mguluchuma -Katavi
Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  ameagiza wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2023  ambao hawaja ripoti shule kwa kukosa sare wapokelewe mara moja shuleni wakati  wazazi wao wanajiandaa kuwatafutia mahitaji yao .

Washiriki Mbalimbali wa kikao kazi cha kuboresha elimu ya Msingi na Sekondary wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wakati akiatoa taarifa ya maendeleo ya elimu ya Msingi na sekondary kwenye Kikao hicho[Picha na Paul Mathias] 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  ameagiza wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2023  ambao hawaja ripoti shule kwa kukosa sare wapokelewe mara moja shuleni wakati wazazi wao wanajiandaa kuwatafutia mahitaji yao .

Vile vile amewaagiza viongozi wote wa Serikali kuanzia wa ngazi za Mitaa ,Vijiji    Kata na Wilaya zote za Mkoa wa Katavi kuakikisha  kuwawasaka wazazi na watoto wa wanafunzi ambao hadi Januari 20 watakao kuwa hawaja ripoti shule.

Mrindoko ametowa maagizo hayo wakati alipokuwa akiwahutubia washiriki wa kikao kazi cha kuboresha ubora wa elimu wa shule za msingi na Sekondari katika Mkoa wa Katavi .

Amesema hadi sasa kati ya wanafunzi Zaidi ya elfu kumi nan ne waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza kwa  2023 ni asilimia 25 ndio wamelipoti .

Hivyo kusiwe na sababu za watoto kushindwa kulipo shule kwa kukosa sare kwa hiyo  kwa   mtoto ambae hajaripoti  shule kwa kukosa sare amepokewe shuleni  hata kama hana sare  za shule na badala yake watumie hata sare walizokuwa wakivaa wakiwa shule ya msingi wakati ambao wazazi wao wanaendelea kuwatafutia mahitaji yao .

Amewagiza viongozi wote wa Serikali katika Wilaya   zote za Mkoa wa Katavi kuhakikisha  wanawasaka wazazi na wanafunzi wa watoto ambao hawajaripoti shuleni wawasake hata kama watakuwa wamejifisha juu ya  miti .

 Mrindoko amewataka  kila mwalimu  azingatie maadili na wawatunze wanafunzi wao  wasiwafanyie vitendo vya ukiukwaji wa maadili .

Kwani wapo baadhi ya walimu wamekuwa na tabia ya kufanya mapenzi na  wanafunzi wao wanao wafundisha  na wengine wamekuwa wakiwafanya wanafunzi wake zao .

Ameagiza walimu wote wanaofanya hivyo waache mara moja  kwani hayo sio maadili  na watakao bainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao .

Katibu  Tawala wa Mkoa wa Katavi Abbas  Hassan Rugwa  amesema kuwa  amesema kumekuwepo  na changamoto  ya  madarasa kwenye shule za msingi  kutokana na ongezeko  la watoto na utolewaji wa elimu bure .

Katibu tawala mkoa wa Katavi Hassan Abbas Rugwa akitoa neno kwa Wajumbe wa
kikao kazi cha Kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondary,ambapo amesema kumekuwa na changamoto ya Madarasa katika ngazi ya Elimu ya Msingi kutokana na Msukumo wa Elimu Bure.[Picha na Paul Mathais]

Ambapo  kwa Mkoa huu madarasa yalipo ni  5,289 huku upungufu wa madara ukiwa ni 3800 hali ambayo inafanya wakati wa masomo wanafunzi  wanakalishwa chini wakati wa masomo ili nafasi ipatikane .

Mkurugenzi  wa usimamizi elimu wa Tamisemi Vicent Kayombo amesema kuwa nia ya TAMISEMI ni kuhakikisha elimu ya shule za msingi na sekondari zinaboreshwa .

Ameeleza kuwa na ndio maana Tamisemi wameitisha kikao kazi hicho  ili kuwepo na uwelewa wa pamoja kwenye kusimamia elimu kuanzia shule za Msingi hadi Sekondari .

kwa habari zaidi  Endelea kutembelea ukurasa wetu wa 

 kataviclub.blogspot.com

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages