Raymond Kanyambo Mratibu wa Mradi wa Shule Bora akitoa Mafunzo kwa waandishi wa habari Mkoa wa Katavi Kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Shule Bora Katika Mkoa wa katavi[Picha na Paul Mathias] |
Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la UKaid kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania limeanza kutekeleza
Mradi wa Shule Bora katika mikoa Tisa Hapa nchini.
Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la UKaid kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania limeanza kutekeleza Mradi wa Shule Bora katika mikoa Tisa Hapa nchini.
Akizungunza wakati wa Semina elekezi ya Kuutambulisha Mradi huo kwa waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi Katika ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Maji Mpanda Mjini .
George Mtawa Msimamizi wa Mradi wa Shule Bora kwa Mkoa wa Katavi Amesema Mradi wa Shule Bora una malengo makuu manne ambayoni Kujifunza, Kufundisha, Jumuishi na Kujenga Mfumo.
Mtawa amesema Kwa ujumla malengo hayo yatakuwa na hakikisho la watoto wa Darasa la awali hadi Darasa la Saba wanasoma hadi Darasa la Saba wanasoma pasipo na mdondoko wa wanafunzi kwenye masomo yao.
Amefafanua kuwa katika mradi wa Shule Bora watahakikisha watoto wote wanakuwa katika mazingira salama na rafiki ili kuwawezesha kuendelea na elimu ya msingi hadi sekondari,
Mradi huo wa Shule Bora umeanza kutekelezwa mwaka 2021-hadi
2027 kwa ufadhili wa serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UK aid utakao
Gharimu kiasi cha paundi za Uingereza Milioni 89 sawa na shilingi za kitanzania
Bilioni 271.
wadau mbalimbali wakiwa katika mafunzo ya utekelezaji wa Mradi wa Shule Bora katika mkoa wa katavi[Picha na Paul Mathias]. |
Amesema wameamua kushirikiana na Kundi la waandishi
wa Habari katika mradi huo kwa lengo la kuyafikia malengo ya utoaji wa
elimu katika mazingira safi kwa wanafunzi wa Awali hadi Darasa la Saba katika ngazi ya shule za Msingi hapa
nchini ikiwemo mkoa wa katavi.
“tumeamua kwa watu wachache ikiwemo waandishi wa
habari kuwa miongoni mwao kwa kuutambulisha Mradi wa Shule Bora kwao
kwa kutambua kuwa vyombo vya habari vinawafikia watu wengi kwa muda
mfupi’’alisema Mratibu Kanyambo
Raymond amebainisha kuwa kufanya kazi na waandishi
wa Habari kuna umuhimu mkubwa kwakuwa wana uwezo katika kupambanua mambo na
kuongea na jamii kupitia Habari, vipindi pamoja na makala wanazoziaandaa kwa jamiikupitia vyombo vyao vya Habari hali itakayosaidia kufikisha ujumbe huo wa Mradi wa Shule Bora kwa ulahisi kwa wananchi.
Waandishi wa habari wa mkoa wa katavi wakiwa katika mafunzo kuhusu Mradi wa shule Bora [Picha na Paul Mathias] |
Kwa upande wake Alex Ngereza Mwandishi wa Habari wa
Radio free afrika na Star Tv ameshauri kuwa na mazingira mazuri ya kikazi baina ya watendaji wa serikali kutokuwa na Mlolongo wa kupata habari kwenye Mradi wa
Shule Bora.
“ unamkuta mtendaji wa Serikali anakubali tatizo
lipo ila anakwambia hili sina mamlaka nalo mpaka nipate kibali toka juu hali
hii huvunja nguvu waandishi katika majukumu yao’’alisisitiza Ngereza
Mradi wa Shule Bora unatekelezwa katika Mikoa Tisa Hapa nchini ambayo ni Katavi,Kigoma,Rukwa,Simiyu,Dodoma,Mara,Pwani, na Singida.
Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi wakiwa katika mafunzo elekezi juu ya utekelezaji wa Mradi wa Shule Bora[ Picha na Paul Mthias] |
Katika hatua nyingine waandishi wa Habari kwa ujumla wamesema mradi huo wa Shule Bora unakwenda kuwa Mkombozi kwa jamii kwa kuisadia serikali katika kuinua kiwango cha Elimu kwa watoto wa Darasa la awali hadi Darasa la Saba kwa shule za msingi katika mkoa wa Katavi na Tanzania nzima kwa ujumla.
Kwa habari zaidi Tembelea katika ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com