UVAMIZI WA VYANZO VYA MAJI HAUKUBALIKI MLELE

 

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akizungmnza na watendaji wa serikali na wananchi baada ya kushiriki kupanda miti kwenye vyanzo  vya maji kwenye Bwawa la Nsekwa lililopo halmashauri hiyo ya Mlele.
[ PICHA na Paul Mathias]
Paul Mathias-Mlele

Wananchi katika halmashauri ya wilaya ya mlele mkoa wa Katavi wametakiwa kutofanya kazi za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji ili kuendelea kuhifadhi vyanzo hivyo.

Mhandisi Girbert Aizaki Meneja wa Ruwasa Mlele akipanda Mti kwenye chanzo cha maji kinacho patikana katika Bwawa la Nsekwa haklmashauri ya Wilaya ya Mlele[Picha na Paul Mathias]
Wananchi katika halmashauri ya wilaya ya mlele mkoa wa Katavi wametakiwa kutofanya kazi za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji ili kuendelea kuhifadhi vyanzo hizo.

Akizungunza mara baada ya kuhitimisha zoezi la upandajimiti katika vyanzo vya Maji kwenye bwawa la Nsekwa lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mlele mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amesema serikali imewekaza fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 2.8 kwaajili ya ujenzi wa mradi huo hivyo vyanzo vyake lazima vitunzwe.

“kwanini tumechagua kuja kupanda miti kwenye eneo hili mnaloliona ni bwawa ambalo Rais Dk Samia Suluhu Hassan ameleta Bilioni 2.8 za kujenga bwawa hili ili tukusanye Maji ya kutosha kwaajili ya wakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele wapatao Sabini na tano elfu”

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akipanda mti kwenye moja ya chanzo cha Maji katika Bwa la Nsekwa halmashauri ya Wilaya Mlele[PICHA na Paul Mathias]
Buswelu amebainisha wale waote waliovamia na kuanza kufanya shuguli zakilimo karibu na kingo na mikondo ya kutililishia maji kuelekea kwenye bwawa hilo waondolewe kwa mazungumnzo ya kuwaelimisha juu ya umuhimu wa vyanzo vya maji na Bwawa hilo kwa ujumla

“Hawa wanaoonekana kufanya kazi kilimo kwenye baadhi ya maeneo ya vyanzo vya maji vinavyotililisha maji kwenye bwawa hili waiteni na muwaelimisha juu ya umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji na muwaeleze umuhimu wa bwawa hili yawezekana hawajawahi kufika na kuliona bwawa hili”amesetitza Buswelu

Amesema mkoa wa Katavi chini ya mkuu wa mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko wamekuja na mpango huo wa upandaji miti mkoa mzima  ili kuhakikisha Mazingira yanatunzwa ikiwemo vyanzo vya Maji kwa masilahi ya vizazi vya sasa navya Baadaee.

Baadhi ya Madiwani Halmashauri ya wilaya ya Mlele wakiwa wamejumuika na wanachi kwenye upandaji miti kwenye vyanzo vya Maji vinavyozunguka Bwawa la Nsekwa.[Picha na Paul Mathias]
Katika kampeni hiyo ya Upandaji Miti iliyofanyika kwa muda wa siku mbili kwenye halmashauri ya wilaya ya mlele Jumla ya miti ipatayo 8896 katika maeneo mbalimbali ikiwemo Shuleni,baadhi ya Maeneo ya Mji wa Inyonga pamoja na maeneo ya vyanzo vya maji vinavyozukunguka Bwawa la Nsekwa.

Kwa upande wake Meneja wa mamlaka ya Usambaji wa maji Vijijini Ruwasa Wilaya ya Mlele Mhandisi Girbert Aizaki amesema wao kama Taasisi ya usambazaji maji vojijini kwa kushirikaina na wadau wengine wa mazingira kwa pamoja wamekuwa na mipango shrikishi kwa kuhakikisha vyanzo vya amaji vinalidwa muda wote.kwa kuwahusisha vijiji vinavyozunguka bwawa hilo.

Wananchi mablimbali na wadau wa mazingira wakiwa katika zoezi la upandaji miti wakipanda miti kwenye chanzo cha Maji kwenye Bwawa la Nsekwa.[PICHA na Paul Mathias]
“tunatoa wito sana kwa wanachi wa vijiji vya Nsekwa,Mtakuja,Wachawaseme,na Kanoge,ili waweze kuwa familia katika utunzaji na uhifadhi wa Bwawa hili kwa sababu,wanapoendelea kulima karibu na Bwawa maana yake watasabisha mmomonyoko wa udongo nakusabisha tope nyigi kujaa kwenye Bwawa hatuta kuwa na tena na bwawana pes azote ziliwekezwa na serikali zitakuwa zimeharibika bure”ameonya Mhandisi Girbart.

Wananchi walioshiriki katika zoezi la kupanda miti kwenye vyanzo vya maji wamesema kuwa hatua hiyo itakwenda kusaidia kulinda hifadhi ya kingo za mito zinazo mwaga maji kwenye Bwawa hilo hali ambayo itakayopelekea upatikanaji wa maji ya kutosha.

Kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages