CCM MPANDA YAHIMIZA KUBUNI MIRADI YA KUKUZA UCHUMI


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi [CCM] wilaya ya Mpanda Method Mtepa akizungumnza na viongozi wa Jumuiya ya wanawake ya chama cha Mapinduzi [CCM] Katika kikao cha kawaida cha Balaza la UWT wilaya ya Mpanda. [PICHA  na Paul Mathias]
Na Paul Mathias-Mpanda

Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda kimeziomba  Jumuiya za chama hicho Wilaya ya Mpanda Kubuni Miradi ya Kiuchumi itakayosaidia kujipatia Kipato na kuepuka kuwa Tegemezi katika utekelezaji wa Majukumu yake ya kila siku.

Mwenyekiti wa chama cha Mpainduzi CCM wilaya ya Mpanda Method Mtepa [wa pili Kushoto ]akiwa na Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mpanda Tausi Ramadhani [wa tatu ]Kushoto  pamoja na Katibu wa jumuiya hiyo [wa wanne  kushoto] Aziza Serf wakiwa katika kikao cha balaza la UWT wilaya ya Mpanda kwenye ukumbi wa mikutano wa chama hicho zilipo ofisi za chama hicho wilaya ya Mpanda.[PICHA  na Paul Mathias]
Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda kimeziomba  Jumuiya za chama hicho Wilaya ya Mpanda Kubuni Miradi ya Kiuchumi itakayosaidia kujipatia Kipato na kuepuka kuwa Tegemezi katika utekelezaji wa Majukumu yake ya kila siku.

Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya ya Mpanda Method Mtepa wakati akihutubia kikao cha kawaida cha Baraza la Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda kilichofanyika Ukumbi wa mikutano kwenye ofisi za chama hicho wilaya ya Mpanda.

Amesema viongozi hao kupitia kamati zao za siasa za Kata wanayo Nguvu ya kuomba miradi mbalimbali ikiwemo Mashamba kupitia kwa viongozi wao wa Vijiji ili kuanzisha miradi ya jumuiya hiyo.

‘’kuna watu mnamashamba huko mlikotoka tunawenyeviti wetu wa vijiji na vitongoji wao ndio wamiliki wakubwa na wasimamizi wa Aridhi hebu waambieni katika vikaovyenu ibua mawazo pale mwenyekiti UWT tunaomba serikali ya Kijiji Itupatie eneo la kulima Karanga na kama kamati ya siasa ikikubali maana yake mambo yanaenda vizuri”

Mtepa amesema kuwa jumuiya hiyo inayouwezo wa kuwaelimisha wanachama na wanajumuiya kuhusu umuhimu wa kuibua miradi ndani ya jumuiya kuanzia ngazi ya kata hali itakayo pelekea kuendelea kujenga uwezo wa kujitemea kupitia miradi hiyo.

Amefafanua kuwa msingi wa maendeleo ya jumuiya ni vikao na mshikamano ili kuyafikia malengo ya kuwatumikia wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM katika jumuiya hiyo na kukifanya chama kiendelee kuamimniwa na wanachi kwakuwa ndicho kinacho tekeleza ilani ya chama hicho kwa sasa kwa ridhaa ya wananchi.

Katika hatua nyingine amewaomba wanachama wa chama hicho kuwa na utamaduni wa kulipia kadi zao za cahama ili kuonesha kuwa wao ni wanachama hai na wasisubirie kukipia ada za uanachama kuelekea nyakati za uchaguzi.

‘’tunalipia kadi zetu wakati wa uchaguzi uongo kweli? waheshimiwa madiwani uongo? Fomu zinatoka ndoa anaanza kujipapasa kulipia ada kwa kuwa kunakipengele kinamtaka afanye hivyo lakini kama hagombei ndo basi tena kwa hiyo kama wewe ni kiongozi hakikisha unailipia kadi yako zaidi yam waka wako wa uchaguzi’"

Katibu wa Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Mpanda Aziza Seirf  amesema kuwa jumuiya hiyo injumla ya wanachama wapatao 9753 na matawi 144 na ongezeko la wanachama ikiwani 471.

Amesema hadi sasa jumla ya wanachama 2285 wa jumuiya hiyo wamesajiliwa katika mfumo wa Tehama ikiwa ni sehemu ya kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia na utandawazi kiutendaji unavyo elekeza ndani ya chama.

Kuhusu kuingiza wanachama wapya Aziza amebainisha kuwa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha January hadi December Mwaka jana wameweza kuingiza wanachama wapya 471

Wajumbe wa umoja wa Jumuiya ya wanawake ya chama cha Mapinduzi CCM  wilaya ya Mpanda wakiwa katika kikao cha kawaida cha Balaza hilo [PICHA NA Paul mathias]
Katika hatua nyingine Katibu huyo amesema kuwa jumuiya inao mkakati wa kuzitembelea kata na kujionea uhai wa Jumuiya hiyo pamoja na kufanya mafunzo kwa viongozi wa kata ili kuwajengea uwezo zaidi wa kiutendaji.

Maria Magesa miongoni mwa wajumbe waliohudhuria Baraza hilo amesema uibuaji wa miradi katika jumuiya itakwenda kusaidia usitawi wa jumuiya hiyo na kuinua uchumi wa wanawake’’miradi ni sawa inaweza kutusaidia kuinua uchumi wetu sisi wanawake lakini miradi tunaipata vipi tukipewa kama mashine za kusaga zitatusaidia kuinua uchumi wetu”

Magesa amaesema umoja na mshikamano ndio sialaha ya ushindi kwa cahama hicho kwakuwa jumuiya hiyo ndio Dira kwa chama hicho kwa kuwa na kundi kubwa la wapigakura hasa wanawake.

Mwanahamisi Amani mjumbe wa kikao hicho amebainisha kuwa hawatamwangusha mwenyekiti wao katika kuibua Miradi ndani ya jumuiya hiyo kwa kuwa kunaabaadhi ya kata zimeanza kuandaa miradi yao na vikundi mbalmbali vya kiuchumi vilivyoanzishwa na akina mama.

Amesema niwakati muafaka sasa kwa wanawake wa jumuiya hiyo kujituma na kufanya kazi kwa bidii kwa kukiendeleza chama na kuyafikia malengo yaliyokusudiwa.

Kwa habari zaidi endelea kutembelea  ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages