VYAMA VYA USHIRIKA KATAVI KUTOKOMEZA HATI CHAFU

 



Washiriki wa mafunzo kutoka vyama mbalimbali vya ushirika  Mkoa wa Katavi wakiwa kwenye Mafunzo kuhususu uandaaji wa taarifa za fedha na utunzaji wa kumbukumbu kwenye vyama vyao[ Picha na Paul Mathias]

Na Paul Mthias- Katavi

Serikali katika mkoa wa Katavi Kupitia ofisi ya Mlajisi imeanza Mkakati wa Kuhakikisha Vyama vya Ushirika vina kuwa na uwezo wa kuandaa taarifa za fedha na kumbukumbu za fedha ili kuepuka Kupata hati chafu au hati zenye mashaka kwa wakaguzi wa Nje.

Mlajisi Msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Katavi Peter Nyakunga akiwahutubia washiriki wa mafunzo kutoka vyama mbalimbali vya ushirika Mkoa wa Katavi[Picha na paul mathias]
Serikali katika mkoa wa Katavi Kupitia ofisi ya Mlajisi imeanza Mkakati wa Kuhakikisha Vyama vya Ushirika vina kuwa na uwezo wa kuandaa taarifa za fedha na kumbukumbu za fedha ili kuepuka Kupata hati chafu au hati zenye mashaka kwa wakaguzi wa Nje.

 Peter Nyakunga Mlajisi Msaidizi wa vyama vya Ushirika mkoa wa Katavi amesema wamefanya mafunzo ya Siku Sita na watendaji wa vyama vya Msingi na wajumbe wa Bodi kwa lengo la kuwajengea uwezo juu ya namna bora ya kuandaa taarifa za fedha na kumbukumbu zake.

‘’nyakunga anasema katika mkoa wetu wa Katavi tulipta taarifa kutoka kwa mkaguzi wa nje vyama vilivyokaguliwa kwa msimu wa Mwaka 2021 katika vyama 34 vilivyokaguliwa hakuna chama hata kimoja ambacho kimeweza kupata hati Safi vyama vyetu vyote vyama 14 vilipata hati yenye shaka tuna vyama 12 vilipata hati isiyo lidhisha tuna vyama 8vilipata hati mbaya ama hati chafu”

Amesema kwa kuliona hilo imewalazimu kufanya mafunzo hayo kwa vyama vyote 47 vilivyopo mkoa wa Katavi kwa lengo la kuhakikisha vyama hivyo vya ushirika vianaondokakana na hali hiyo ya kuwa na hati chafu au mbaya kwenye hoja za ukaguzi wa nje.



“tuliona kuna shida katika utunzaji wa kumbukumbu za chama sasa tukasema mafunzo haya tuite watalamu kuja kutusaidia kutufundisha tuweze kuandika ilea miamala yetu kila siku iweze kukaa vizuri tutunze kumbukumbu zetu za uhasibu vizuri ili tutakapo kwenda kupeleka hesabu zetu kwa mkaguzi hizi hati mbaya tuepukane nazo”

Kwa kipindi hicho cha siku sita wameweza kupitishana na kukumbushana juu ya Misingi ya uendeshaji wa vyama vya ushirika kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo ili vyama hivyo viendelee kuwa imara zaidi katika utendaji kazi.

Nyakunga amewakumbusha viongozi hao wa vyama vya Ushirika kutokuwa sehemu ya migogoro kwenye vyama vyao hali ambayo hudhofisha vyama hivyo katika kutekeleza majukumu yao kwa wanachama.

“tumeweza kuwasaidia ni namna gani wanaweza kusimamia vyama vyao hata inapotokea migogoro juu ya vyama vyao kuweza kushugulikia migogoro hiyo na kuitatua wao kama viongozi wa chama.

Restuta Mussa mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo amesema wamejifunza mambo kadhaa ikiwemo kupitishwa kwenye kanuni za kuujua vizuri ushirika na miongozo yake na watakwenda kuya fanyia kazi yale waliyofundishwa.

“ugumu wa kwanza ambao tulikuwa tunaupata hapo kabla ni elimu tulikuwa hatujapatiwa elimu tunatalajia tukienda kule kwenye chama kitasimama kwa elimu hii” amesema Restuta

Charles Kapamba kutoka chama cha Msingi Ilunde amesema mafunzo hayo yanakwenda kuwa chachu katika kuhakikisha chao kinafanya vizuri katika masuala ya ukaguzi kama yalivyo fundishwa.

“kabla ya mafunzo hayo tulikuwa na changamoto nyingi kunawakati inafika unampgia simu afisa ushirika akuelekeze jammbo Fulani lakina kwa sasa hivi baada ya kupata mafunzo haya naaamini mambo mengi kimsingi yatakenda vizuri”

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages