ASIKARI UHAMIAJI ATUHUMIWA AJALI YA BODABODA


wakazi wa Kijiji cha Milala wakiwa katika mazishi ya Dreva Bodaboda Marehemu Alex Lutana alifariki kwa Ajali [Picha na George Mwigulu]

Na Paul Mathias- Katavi

Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Milala Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wamewatuhumu Asikari wa Jeshi la uhamiaji kwa kusabisha kifo  cha Mwendesha Bodaboda kwa Kugogwa na Bus la Adveture wakati wakimfukuza kwa kumshakia kuwa alikuwa amebeba  raia wa kigeni.

waombolezaji katika msiba wa Boda Boda alex Lutana wakiwa eneo la makaburi kijijini Hapo[ Picha na George Mwigulu]

Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Milala Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wamewatuhumu Asikari wa Jeshi la uhamiaji kwa kusabisha kifo  cha Mwendesha Bodaboda kwa Kugogwa na Bus la Adveture wakati wakimfukuza kwa kumshakia kuwa alikuwa amebeba  raia wa kigeni.

Wananchi hao wakiongea mbele ya wandishi wa habari  wamebainisha kuwa ajali hiyo imesabishwa na asikari hao wakati wakimfukuza Mwendesha Boda boda aitwaye   Alex Lutana na Gibson Mkatakona ambae ni Majeruhi kwa kile walichokuwa wanadai alikuwa amebeba wahamiaji haramu.

Philipo Kachila mkazi wa kijiji cha Milala amesema kuwa kijana huyo akiwa anatokea kijijini hapo alipofika eneo la ukaguzi  wa kuwabaini wahamiaji haramu alianza kufukuzwa na asikari hao kwa kutumia gari lao bila kujua kiini cha kumfukuza na ndipo katika harakati za kuwakwepa ndipo Bus hilo likiwa mwendokasi na kumgonga na kufariki Dunia hapo hapo .

‘’Wakati Bus la Adveture linakaguliwa boda huyo alipita akiwa amebeba watu wawili baada ya kuwa amepita hapo wale asikakari wa uhamiaji walidhani amebeba wahamiaji haramu ndipo walianza kuwafukuza hadi eneo la Milupwa Marehemu akiwa katika  kuwakimbia askari hao  inadaiwa alivutwa shati  hari ambayo  ilimfanya   Bodaboda kuhaamia upande wa pili wa barabara  na ndipo alikutana na Bus la Adveture na kumgonga ’’amesema kachila

 Kwa upande wake Thomas Mtolezi mkazi wa Milala amesema mnamo majira ya saa saba mchana walipata taarifa ya kifo cha Boda boda huyo hali ambayo iliwashitua na kuwalazimu kufika eneo la tukio eneo la Milupwa.

Ndipo walipokuta ajali hiyo imetokea chanzo kikiwa ni kufukuzwa Bodaboda huyo na askari  wa uhamiaji.

‘’tulipata taarifa hii majira ya mchana tukio ambalo limetusikitisha wanakikiji wa Milala kuna Boda boda  mkazi wa Kijiji ca ha Milala alikuwa amebeba watu wake toka Milala kuja nao Mjini lakini baada ya kufika eneo ambalo Asikari walikuwa wanalifanyia ukaguzi Bus la Adveture wakahisi Boda bod huyo amebeba wahamiaji Haramu matokeo yake wakaanza kumfukuzia walipofika milupwa ndpo asikari huyo wa uhamiaji akiwa kwenye gari lake alifungua Dirisha na kumfuta shati Boda boda huyo bodaboda huyo alitaka kugeuka upande wa pili ndipo allgongwa  na Bus la Adventure na kusabisha kifo cha Alex Lutana amabe ni Mwendesha Boda Boda’’

Kwa wake shemeji  wa Malehemu Kabona Gibson Mkazi wa Milala amebainisha kuwa alipata taarifa ya ajali hiyo majiara ya saa nne asubuhi na kwenda eneo la ajali hiyo ndipo alipokuta ndugu yake akiwa amefikwa na umati na mwenzake akiwa amejeruhiwa vibaya.

Katika hatua nyingine wananchi hao wamesema kuwa tukio hilo litakuwa la mara ya pili kwani kuna tukio la aina kama hilo la bodaboda kufukuzwa na Asikari wa uhamiaji lilitokea ingawa halikusabisha kifo.

Wakazi wa kijiji cha Milala wakielekea eneo la Makaburi kwaajili ya mazishi ya Dreva Boda Boda Alex Lutana alifariki Dunia kwa ajali ya Barabarani [Picha na George Mwigulu]
Marehemu Alex Lutana amezikwa katika Kijiji cha Milala huku Majeruhi wa ajali hiyo Gibbson Mkatakona akiwa anaendelea kupatiwa Matibabu katika hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi na hali yake ikiendelea kuimarika

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame amekili kutokea kwa kifo hicho na kuahidi kutoa taarifa zaidi juu ya tukio hilo baada ya uchunguzi wa kina kufanyika.

‘’nikweli imetokea hiyo ajali nyakati za mchana ililipotiwa kwamba huyo kijana wa Boda Boda alipita hapo aliposimamishwa na watu wa uhamiaji hakutii lile agizo na kukimbia huku akiwa na mashaka akiwa katika hali ya kugeuka ndipo alipokutana na ajali hiyo na kuingia uvunguni na hayo nimatokeo ya Boda boda kukataa kusimama kwenye eneo la ukaguzi” amesema kamanda Makame.

Kuhusu uwepo wa mkimbizano baina ya Asikari hao na Bodaboda huyo kamanda makame wanaendelea kufanya uchunguzi juu ya hilo na watatoa taarifa kwa umma.

‘’tukishasema tunachunguza maana yake yote hayo tutakuja kuyabaini lakini kwanza turipoti hilo kama tutabaini kunajambo jingine basi hatutasita kuendelea kutoa taarifa juu ya hilo’’

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages