CCM : KATAVI YA MWANGUKIA RAIS SAMIA JENGO LA DAMU SALAMA

 

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Idd Kimanta akizungumnza ofisini hapo alipotembelelewa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiwa katika zaiara ya kikazi mkoani katavi[Picha na Paul Mathias]

Na Paul Mathias.Katavi

Chama cha Mapinduzi CCM katika mkoa wa Katavi  kimeipongeza serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha miundombinu Katika sekta ya Afya kwa vitendo.

Waziri wa Afya Ummy mwalimu katikati mwenye kilemba Cha njano  akiwasili katika ofisi za chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi[Picha na Paul Mathias]

Chama cha Mapinduzi CCM katika mkoa wa Katavi  kimeipongeza serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha miundombinu Katika sekta ya Afya kwa vitendo.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi Idd Kimanta wakati akitoa salamu za chama kwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alipotembelea ofisi za chama hicho amesema pamoja na serikali kuleta Miradi Mingi lakini kumekuwa na changamoto ya vifaa tiba kwa watalamu wa afya hali ambayo hupelekea wanachi kuto pata huduma za uhakika

‘’lakini tunawatalaamu hapa,tuna mtaalamu wa Masikio pua na koo bingwa anae bobea Mh waziri hana vifaa tunae daktari bigwa wa Cmt yupo hapa anapata mshahara lakini tunae daktari wa Bingwa wa hanavitendea kazi sasa ukiwa na watu wa aina hiyo amamabao ni wasomi katika fani zao wakawa hawako bize inaleta shida lakini pia hatuna Daktari bingwa wa watoto kwa mkoa wa Katavi hatuna’’

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akisoma taarifa mbalimbali ya utekelezaji wa miradi ya afya katika mkoa wa Katavi alipotembelea ofisi za chama chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa katavi ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani Katavi.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo ameiomba serikali kuaona namna ya kujenga kituo cha kuhifadhia damu katika mkoa wa Katavi ili kupunguza usumbufu kwa wa kupeleka damu katika mkoa wa Tabora ambayo imekuwa chanzo cha vifo kwa wananchi kwa kuchelewa kupata huduma ya Damu.

‘’ukitoka hapa kwenda Mwanza ni kilomita zaidi ya 700 ukitoka hapa kwenda Rufaa Mbeya ni kilomita 580 utaona nikwanamna gani sisi hapa tulipo tunamatizo makubwa katika kupata huduma za juu kidogo ombi kwanza umfikishie Rais ombi la wanakatavi tunamuomba sana Mh Rais atujengee jengo la Damu salama sasa hivi sasa tukikusanya damu inaenda kusafishwa Mkoa wa Tabora kuna akina mama wajawazito wakipata kifafa cha Mimba kakma hakuna damu inakuwa tatizo kwahiyo tunamuomba Rais atusaidie jengo la damu salama’’amesema kimanta

Katika hatua nyingine amesema kujengwa hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi inakwenda kuwa Mkombozi kwa utoaji wa huduma za matibabu kwa wanachi wa mkoa wa Katavi.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema kuwa serikali imechukua ombi la kujenga kituo cha damu salama katika mkoa wa Katavi pamoja na mpango wa serikali wa kujenga hospitali ya Kanda mkoa wa Kigoma ili kulahisisha upatikanaji wa Matibabu kwa wanachi wa mkoa wa Katavi.

Viongozi mbalimbali wa chama na serikali katika mkoa wa Katavi wakiwa ofisi za chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi wakati waziri wa afya Ummy mwalimu alipotembelea ofisi za chama hicho Mapema leo[Picha na Paul Mathias]

‘’lakini nazani kwa asili ya mkoa wa Katavi kwenye mipango yetu kwa mfano MRY siyo lazima mtu aende Kigoma tutaangalia kwa asili yake kwahiyo tunaweza tukaweka utilize moja baada ya nyingine dayalisisi nazani huduma zitaanza kutolewa mara tumeanza na hospitali za rufaa kumi hii ya EAT nimeipokea moja’’amesema Waziri Ummy

Amesema serikali ya mkoa kwa ujumla iendelee kuwatunza watendaji wa afya kwakuwa wanafanya kazi ya kuokoa uhai wa wananchi pamoja na changamoto kadhaa zinazo wakabili na serikali ikiwa inaendelea kutatutua changamoto hizo kwa kadri  inavyowezekakana.

 Kwa habari zaidi Tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages