UTOAJI WA CHAKULA SHULENI KUTOKOMEZA UTORO


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli akiwa ofisini kwake wakati wa mazungumzo na chomo hiki kuhusu utekelezaji wa Mpango wa utoaji wa chakula Shuleni kwa wanafunzi Picha na Paul Mathias]

Na Paul mathias ,Mpanda

Halmsahauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi imeweza kutekeleza Mpango wa utoaji wa chakula Shuleni kwa shule za Msingi na Sekondari kwa asilimia 85.3 na  kuongeza Chachu ya ufaulu kwa wanafunzi.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli akizungumnza namana halmashauri yake inavyotekeleza mpango wa chakula Shuleni kwa wanafunzi [Picha na Paul Mathias]

Halmsahauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi imeweza kutekeleza Mpango wautoaji wa  chakula Shuleni kwa shule za Msingi na Sekondari kwa asilimia 85.3 ili kuongeza Chachu ya ufaulu kwa wanafunzi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli amebainisha hayo wakati akizungumnza na chombo hiki namna halmashauri hiyo inavyotekeleza agizo la Sera ya Elimu kuhusu utoaji wa chakula Shuleni.

Kumbuli anasema’suala la Chakula katika Sera ya Elimu tunalitekeleza katika shule zetu hizi zote ambapo tukifanya shule za msingi na sekondari tunakuwa na jumla ya shule 68 kati ya hizi shule, shule 58 na kati yake hapo Shule za msingi 43 na 15 za sekondari zinatoa hicho chakula na hivyo basi kutupa idadi hiyo ya shule 58 na kuwa na  asilimia 85.3’’

 Amebainisha kuwa wanaendelea na Kampeni ya kuhasisha jamii kupitia kwa wazazi wafahamu umuhimu wa Mpango wa chakula Shuleni kwa lengo la kutimiza lengo la Asilimia Miamoja katika kutekeleza mpango huo kwenye manispaa ya Mpanda kwa lengo la kuwa na ufaulu ubora kwa wanafunzi kwa unaotokana na msukumo wa utoaji wa chakula Shuleni.

‘’tunafanya hivyo kwa sababu bila chakula inaamaana hakuna amabae anaweza akafanya masomo kuwa vizuri na hivyo kupitia kutolewa kwa chakula hawa wazazi amabao jukumu hili liliachwa kwao ikiwa ni pamoja na chakula na Sare pamoja na Daftari ambalo wanalitimiza kwa kiasi kikubwa kiukweli basi linapelekea kuinua ufaulu wa shule hizo za msingi na sekondari kwa mfano shule za Msingi matokeo ya Darasa la Saba yalikuwa asilimia 87 lakini na sekondari zaidi ya 87 haya yote ni matokeoa ya watoto kupata chakula shuleni’’

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli akiwa ofisini kwake 
Amesema wamejiwekea mkakati kupitia Bodi za shule na kamati za shule kuhakikisha zoezi hilo linakuwa endelevu kwaajili ya usitawi wa elimu kwa kushirikiana na wazazi kupitia kamati hizo wa kuhakikisha chakula kinatolewa shuleni.

Kuhusu hali ya uripoti wa wanafunzi wa Kidato cha kwanza 2023 hadi sasa kwenye halmsahauri ya Manispaa ya Mpanda umefukia asilimia 92 huku asilimia nane iliyobakia wakiwa wametoa maelekezo kwa watendaji wa kata na mitaa kupita nyumba kwa nyumba ili kuwabaini wale wote ambao hadi sasa hawajaripoti shuleni.

‘’nitoe rai kwa watoto kuna asilimia 8 wa shule za sekondari tuliotegemea ili wafikishe asilimia miamoja ya kuripoti wale form One mpaka sasa hivi tuna asilimia hiyo 92 na hii asilimia nane tayari jana tumetoa maelekezo kwa watendaji kuhakikisha wanapita nyumba kwa nyumba kuwaibua hawa watoto kwenda shuleni “ameeleza Kumbuli

Kila mzazi ana wajibu wa kuhakikisha anaungana na serikali katika kuunga mkono mipango mbalilimbali katika sekta ya elimu ili kuimalisha ubora wa Elimu Hapa nchini kwa kutengeneza mazingira wezeshi kwa watoto ikiwemo kuhakikisha wanakuwa sehemu ya mpango huu wa utaoaji wa chakula Shuleni. 

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com Endelea kuwa nasi

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages