TAYOBECO YAJA NA MRADI WA WANAWAKE NA VIJANA


Mkuregenzi Mkuu wa  shirika lisilo la kisrikali la  TAYOBECO     Shida  Kabulunge  akiwatubia wadau mbambali  kabla ya kuzinduliwa kwa mradi wa  Boresha Habari 

 

Na Waltre Mguluchuma,Katavi 

Shirika la  lisilo la Kiserikali la Tanzania Behavioural Change Organization TAYOBECO limezindua Mradi wa Boresha habari wenye lengo la kuhamasisha  vijana na wanawake juu ya umuhimu wa Kupata Chanjo ya UVIKO 19 na chanjo mbalimbali katika Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi kwa udhamini wa INTERNEWS ili watu waweze kuwa na afya Bora.

Baadhi ya washiriki wa Mradi wakiwa katika Picha ya Pamoja

Shirika la  lisilo la Kiserikali la Tanzania Behavioural Change Organization TAYOBECO limezindua Mradi wa Boresha habari wenye lengo la lkuhasisha vijana na wanawake juu ya umuhimu wa Kupata Chanjo ya UVIKO 19 na chanjo mbalimbali katika Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi kwa udhamini wa INTERNEWS ili watu waweze kuwa na afya Bora.

Mradi huu utakuwa ni mkombozi mkubwa katika kuboresha afya za wananchi wa Mkoa wa Katavi kwa kuanzia kwa watoto ,Vijina na Wazee.

Mradi huu  umezinduliwa kwenye  ukumbi wa Kichangani ulipo kwenye Mtaa wa Nsemlwa Manispaa ya Mpanda ambao wadau mbalimbali walishiriki kwenye uzinduzi huu.

Mkurugenzi  Mtendajiwa  TOYOBECO   Shida  Kabulunge  amesema shirika hilo  lisiro la Kiserikali  hapa nchi ni lilianzishwa mwaka wa 2019.

 Amebainisha kuwa kutokana na utafiti uliofanywa  hivi karibuni imebainika kuwa Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa mine ambayo imekuwa na mwitikio  mdogo kwenye maswala ya chanjo pamoja na mikoa ya Kigoma ,Njombe na Simiyu hivyo ndio maana wameona kuna haja ya kutowa elimu kwenye Mkoa wa Katavi .

Shirika hili  mwaka 2020/2021 walitowa elimu  ya matumizi sahihi  ya dawa  mpya  za kufubaza  maambukizi ya UKIMWI  Tenofovir,Lamivudine  Dolutegravir Ltdkwa Mkoa wa Dar salaam kwa kipindi cha mwaka mmoja na  310 PLHIV walirudi kwenye dawa .

Kabulunge amesema kuwamradi wao watatu  wa kutowa  elimu ya matumizi  salama  ya  mitandaoni ,ukiwa  na lengo  la kukomea  na kuelimisha  jamii juu ya ukatili  wa kijinsia  mitandaoni  ambao ulifadhiliwa na  Shirika  la Zaina  Foundation Tanzania  watumiaji 95 mitandaoni waliweza kufikiwa .

Meneja wa   programu wa TOYOBECO    Adinani    Mussa   akielezea namna ya mradi wa Boresha Habari utakavyo fanya kazi katika Mkoa wa Katavi kwa kuwahamisisha vijana na wanawake juu ya chanjo ya UVIKO 19 wakati wa uzinduzi wa mradi huu uliofanyika katika ukumbi wa Kichangani Manispaa ya Mpanda

 

Hivyo   mwezi oktoba mwaka jana  Internews walitowa ombi  la kutaka taasisi  ziombe  sehemu ndogo  ya mradi  huu ili ziweze  kutekelezwa  katika maeneo mbali mbali ya Tanzania na wao  TOYOBECO wakachangua Katavi.

Mradi huu  wa Sai  Boresha Habari  ulikuwa na  malengo  mbambali  kiliwemo lengo ambalo wamelizindua  kwenye mradi huu katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi .

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages