DC : JAMILA MUWASA FATILIENI MKATABA MRADI WA MAJI MIJI 28


Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akifunga kikao cha kamati ya ushari DDC Wilaya ya Mpanda

Na Walter Mguluchuma

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameiagiza Mammlaka ya Maji na usafi wa Mazingira Mpanda Muwasa kufatilia kwenye mamlaka zinazo husika ili mradi wa Maji wa Miji 28 katika Bwawa la Milala uanze kutekelezwa ili kutatua kero ya Maji kwa wananchi.

Viongozi wa serikali na chama Serikali wakiongozwa na Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph wakiwa katika kikao cha ushauri cha wilaya ya Mpanda DCC

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameiagiza Mammlaka ya Maji na usafi wa Mazingira Muwasa kufatilia kwenye mamlaka zinazo husika ili mradi wa Maji wa Miji 28 katika Bwawa la Milala uanze kutekelezwa ili kutatua kero ya Maji kwa wananchi.

 Maagizo hayo ameyatoa wakati akifunga kikao cha kamti ya ushauri ya Wilaya DCC kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mpanda Social Hall amesema tayari mikataba hiyo imesainiwa na Viongozi wetu wa juu hivyo nijukumu la mamlaka kufatilia utekelezaji wa Mkataba huo kwani Mji wetu wa Mpanda nimiongoni wa wanufaika wa mkataba huo kupitia Bwawa la Milala.

 ‘’mkataba ule uliposainiwa ilitakiwa January tuanze kuona mkataba ule unatekelezwa kwa hiyo nitumie nafasi hii kuwaagiza Muwasa habari ya kukaa hapa na kuandika barua na kusubilia wizara si imefanyaje mfatilie Mradi uanze Mh Rais alishuhudia utiaji saini huo katika mkataba huo wa miji 28 ikiwemo mji wa Mpanda jukumu letu kama viongozi kumsaidia  Rais katika majukumu yetu kwa hiyo Muwasa mfatilie mradi huu uanze’’amesema Jamila

Watumishi mbalimballi wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya Nsimbo wakiwa katika kikao cha ushauri wilaya ya Mpanda

Jamila amebainisha kuwa kwa mujibu wa Mkataba huo ilitakiwa uanze kutekelezwa Mwezi janury na Mpaka sasa hakuna Mkandarasi alieingia kwenye eneo la Mradi huo hali ambayo inawafanya viongozi kushidwa kuelewa tatizo lipo wapi

‘’janury imeshakatika na sasa tupo February na inakaribia katikati mkandarasi haonekani eneo la Mradi na hatujui kitu gani kinaendelea pale kwa hiyo Muwasa mfatilie mradi huo kwa wizara tunataka mradi unaze kutekelezwa’’

Katika hatua nyingine ameziagiza Taasisi za serikali kuhakikisha zinapokuwa kwenye vikao mhimu kama DCC kuwa na taarifa sahihi kwakuwa kikao hicho kina malengo makubwa ya maendeleo ya Wilaya ya Mpanda.

Viongozi wa dini pamoja na wakuu wa Taasisi wakiwa katika kikao cha ushauri cha Wilaya ya Mpanda.
‘’zipo taasisi ambazo hazijawasilisha taarifa  hapa bajeti zao ilitakiwa ziwasilishwe na zizungumnze hapa wanatalajia kufanya nini kwa hiyo hizi nipate maelezo kwamba nikwa nini taarifa zao hazijawasilishwa hapa’’

Jamila yusuphu amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha katika sekta  ya Elimu ambapo wilaya ya Mpanda imepokea kiasi cha Shilingi Bilioni 1 na milioni 500 ambazo zimetumika kujenga Mdarasa 78 kwaajili ya kujenga Madarasa kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2023.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wilaya ya Mpanda Keneth Pesambili amesema kwa upande wa halamshauri mbili za Manispaa ya Mpanda na Nsimbo kwa taasisi za Tarula,Muwasa na Ruwasa zimewasilisha mapendekezo ya Bajeti yenye kiasi cha Shilingi Bilioni 64 .1 kwaajili ya bajeti kwa Mwaka 2023/2024.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages