Na Paul Mathias-KTPC Katavi.
Wanafunzi wa Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Nsemlwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa katavi wametembelea ofisi za Chama cha waandidhi wa Habari Mkoa wa katavi kwa lengo kujionea namna habari zinavyoandaliwa na kuchakatwa kabla ya kuchapishwa na kurushwa katika vyombo mbalimbali vya habari
Wanafunzi wa Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Nsemlwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa katavi wametembelea ofisi za Chama cha waandidhi wa Habari Mkoa wa katavi kwa lengo kujionea namna habari zinavyoandaliwa na kuchakatwa kabla ya kuchapishwa na kurushwa katika vyombo mbalimbali vya habari.Wanafunzi wa shule ya sekondari Nsemlwa wakiwa katika ofisi za chama cha waandishi wa Habari mkoa wa Katavi.
Wanafunzi hao wamesema kuwa
wamejifunza juu ya umuhimu wa vyombo vya habari na waandisahi wa habari namna
wanavyo ipasha habari jamii kwa kutumia vyombo vyao vya habari.
wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nselwa wakiwa na Mwandishi wa Habari Irene Temu wa uhuru Media katavi |
Nikuda Mashaka mwanafunzi wa Kidato cha Nne Shule ya Sekondaeri Nsemlwa amebainisha kuwa amejifunza kuwa vyombo vya habari vinamchango mkubwa katika ukuzaji wa lugha ya Kiswahili kwakuwa vyombo vya habari kupitia waandishi wa habari hutumia lugha ya Kiswahili kwa ufasasaha kwa wananchi.
‘’nimeona umuhimu wa habari tunapata habari mbalimbali ambazo tulikuwa
hatujui tunazipata kupitia waandishi wa habari tunaweza kueneza Kiswahili kwa
kutumia vyombo vya habari ‘’amesema Nikuda.
Amesema kuwa katika ulimwengu huu
wa Sayansi na Technolojia amejifunza namna ambavyo vyombo vya habari
vinakabiliana na maendeleo hayo ya Utandawazi kwa kuendaana na soko na
mazingira yaliyopo.
Kwa upande wake Kiliani Jonh
Mwanafunzi wa Kidato cha Nne Nsemlwa Sekondari amesema kuwa vyombo vya habari
alivyojifunza vinamchango katika ukuaji wa uchumi kupitia habari mbalimbali za
kibiashara na masuala ya kiuchumi.
‘’Vyombo vya habari vinaumuhimu
kwa sababu vinakuza lugha yetu na vilevile vinaweza kuchochea ukuaji wa uchumi
wa Nchi kupitia taarifa mbalimbali za mambo ya kiuchumi’’ amenena Kiliani
Sadiki Donald ambae alikuwa
sehemu ya wanafunzi waliofika katika ofisi za chama cha waandishi wa Habari
mkoa wa katavi ameeleza kuwa ametambua kuwa jukumu kubwa la vyombo vya habari
kuelimisha,Kuasa, na kukosoa pale inapobidi kama kuna mkanganyiko wa Jambo fulani
katika jamii lenye Masilahi kwa umma ili
serikali kuchukua hatua za kiuwajibikaji kwenye jambo husika
Wanafunzi wa kidato cha Nne Nsemlwa Sekondari wakipatiwa uelewa juu ya uandishi wa habari |
Katika hatua nyingine Walter
ametoa wito kwa Wanafunzi wa shule nyingine katika mkoa wa Katavi kuja katika ofisi hizo kwa kuwa miongoni mwao
niwana habari wa siku zijazo
kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com