KIMANTA : SERIKALI IMARISHENI BARABARA VIJIJINI


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Iddy Kimanta akiwa hutubia wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM katika maadhimisho ya Miaka 46 ya kuzaliwa kwa chama hicho yaliyofanyika kijiji cha Katuma wilaya ya Tanganyika.[Picha na Alex Ngereza]
Na Alex Ngereza -Katavi

Katika kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi Iddy Kimanta amemwagiza mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kuakikisha barabara ya Karumbi kwenda Kabatini katika kata ya katuma inatengenezwa.

Gilbert Sampa MNEC kutoka mkoa wa katavi akiwa na mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Mrindoko wakiwa katika ukaguzi wa Miradi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 46 ya kuzaliwa kwa CCM[Picha na Alex Ngereza]

Katika kuadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi Iddy Kimanta amemwagiza mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kuakikisha barabara ya Karumbi kwenda Kabatini katika kata ya katuma inatengenezwa.

Akitoa maagizi hayo Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi Kimanta baada ya chiefu Malaki kuomba kauli ya chama kutokana na maeneo hayo kuwa kitovu cha kuzalisha tumbaku lakini pamoja na fedha nyingi ambazo zimekuwa ziingia kutoka kijiji hicho baada ya kuuza tumbako lakini miundombinu ya barabara imekuwa mibovu na haipitiki ndipo Mwenyekiti akamuagiza Mkuu wa mkoa wa katavi kuimaliza changamoto hiyo kwa kufanya matengenezo.

Katika Mkutano huo Mwenyekiti alilazimika kutoa maagizo Kwa mkuu wa mkoa kwa mara nyingine baada ya kikundi cha upendo kilichopo kijiji cha Karubi katuma kuomba kupatiwa mashine ya kujamua mafuta ambayo wameiomba muda mrefu lakini bado kumekuwa na changamoto akamuagiza Mkuu wa mkoa kuhakikusha wanakikundi hao wanapatiwa mashine haraka iwezekanavyo. Nataka hawa akina mama uwapatie mashine leo leo unafanyaje mimi sijui itakuwaje mimi sielewi chamsingi hawa wanawake wapewa mashine pamoja na mafunzo ya namna ya kuendesha hiyo mashine.

Chief Mallak akitoa hoja ya kujengwa kwa barabara ya Kirubi Kabatini [Picha na Alex Ngereza]
Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amekuri kuyapokea maagizo hayo huku akieleza kuwa barabara ya kwenda kabatini imetengewa bajeti tayari shilingi milioni 200 kwa ajiri ya kuanza matengenezo Aidha amesema swala la kikundi cha Upendo kukopeshwa amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kikundi kipatiwa mashine haraka iwezekanavyo.

katika utekelezaji wa ilani mjumbe wa halmashauri kuu Taifa CCM Mkoa wa Katavi Gilbart Sampa ameeleza kuwa Ilani ya CCM ndani ya Mkoa wa katavi imetekelezeka kwa kiwango kikubwa upande wa vituo vya Afya  barabara, maji, Elimu na sekta mbalimbali huduma zimewafikia wananchi na bado cha Mapinduzi kinaendelea na kitaendelea kuisimamia Serikali ili iendelee kufikishia maendeleo Wananchi.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa Mwanamasudy Pazi amesema kwa kipindi hiki kifupi chama hicho kimepata mafanikio makubwa kwa kuwaingiza Wanancha wapya kwa mfumo wa kielektroniki ambao ingizo jipya ni zaidi ya Wanachama 2700

Chalres Malack ni mmoja wa viongozi na mkazi wa eneo la kijiji cha Karubi kabatini amekiomba chama cha Mapinduzi kutoa tamko kuhusu barabara yao kutoka na vijiji hivyo kuwa kitovu cha uzalishaji wa zao la Tumbaku ambapo amesema kwa mwaka mzima huingiza zaidi ya bilioni moja na kwa mwaka huu tunaweza kuzalisha zaidi ya hizo kwa hali ulivyoiona ya njia yetu mwenyekiti tunaomba utoe tamko ili na sisi tupate neema ya ilani ya chama chetu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages