VIJANA KIKWAZO MAREJESHO FEDHA ZA HALMASHAURI


Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi Halima Kitumba akizungumzia mwenendo wa utoaji wa mikipo kwa Vijana [Picha na Paul Mathias]

Na Paul Mathias-Tanganyika

 Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika mkoa wa katavi imeanza kutekeleza Mpango wa kutoa vifaa vya kazi kwa vijana kupitia asilimia nne za mapato ya ndani kama sheria inavyo elekeza .

Hayo yamebainishwa na Halima Kitumba Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakati akizungungumnza katika zaiara ya Mjumbe wa Baraza wa UVCCM Taifa mkoa wa Katavi Mhandisi Debora Joseph alipotembelea ofisi hiyo ili kujua mwenendo wa utoaji wa mikopo kwa vijana.

Akito taarifa hiyo Kitumba amesema kuwa wamekuwa wakitoa Mikopo hiyo kwa vijana kwa kadri ya Mashart yaliyopo huku miongoni mwavijana hao wakiomba vifaa saidizi vitakavyo saidia kuendesha Miradi yao kwenye baadhi ya maeneo ya halmashauri hiyo.

‘’hili suala tuliagizwa kitaifa na mama Samia tangu akiwa makamu wa Rais na tunalifanyia kazi ukienda Kasekese nina kikundi cha vijana ambacho kina chakata mafuta ya Alizeti tuliwapa mashine pia ninakikundi kingine ambacho kinachakata unga wa sembe tuliwapa Mashine’’ amesema Halima

Pamoja na hayo ameeleza kuwa vijana katika kijiji cha Kasekese wamewezeshwa fedha hizo za vijana kwa kuanzisha Ghala lakuhifadhia nafaka pamoja na ghala la kuhifadhi nafaka katika kijij cha Kamsanga .

‘’kuna mkopo ambao tumewapa mwaka huu wa fedha robo ya kwanza kuna Ghala limejengwa Kasekese tuna Maghala Kamsanga tunajitahidi lakini wengine wanakuja na wazo wanakuambia sisi tunafanya biashara ya kukusanya Mazao kama ni Mazao lazima umpe Cash kwahiyo wanaotaka vifaa huwatuwapa kipaombele’’ ameeleza Kitumba

Amesema kikwazo kikubwa kwa Vijana imekuwa ni kutolejesha Fedha hizo  kwa wakati hali ambayo imekuwa inawapa changamoto kutoa fedha hizo kutokana na fedha kuoonekana kwenye vikundi hivyo lakini katika uhalisia fedha hizo hazionekani kwa kutokulejeshwa.

‘sasa hivi tu jamani naomba msituingilie tunakwenda Mahakamani kwa vijana vijana wekuwa ni tatizo wamekuwa na tamaa kwa takwumu za sasa hivi kuna milioni 318 zipo kwa vijana tangu mwaka 2009 nasijui nazipata wapi ameeleza afisa huyo’’

Amebainisha kuwa kwa Robo ya kwanza tayari wametoa Shilingi Milioni 125 kwa vijana kama sehemu ya Asilimia nne kwa vikundi vya vijana

Masunga Magaka mkazi wa Kapala Msenga ambae ni kijana anasema suala la Mikopo limekuwa likiwapa changamoto kutokana na baadhi ya vijana kuchukua mkopo na kushidwa kurejesha na wao kukosa fursa hiyo.

‘’kila tunapomba hii mikopo tunaenda tunaambiwa kuna vijana ambao wamekopa ila hawajarudisha kwa mfano hapa kapala msenga hakuna vijana waliopatiwa mikopo’’

Nae Aisha Rashi Mkazi wa Kijiji cha Katuma anasema fursa hii ya mikipo kwa vijana ni nzuri inawakwamua vijana ingawa vijana wamekuwa wakipata changamoto kwenye miradi wanayo iibua kwenye maeneo yao.

Kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

Kataviclub.blogspot.com 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages