MADIWANI TANGANYIKA KUHAMASISHA WANAFUNZI KWENDA SHULE



Mweyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi Hamad Mapengo akiongoza kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani[Picha na Paul Mathias]
Na Paul mathias- Tanganyika

Madiwani katika halamsahauri ya wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameombwa kuwa mabalozi kwa wananchi kwenye kata zao kufanikisha wanafunzi walio chaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanakwenda kauanza masomo swhemu walizopangiwa.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakiwa katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani [Picha na Paul Mathias]
Madiwani katika halamsahauri ya wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameombwa kuwa mabalozi kwa wanamchi kwenye kata zao kufanikisha wanafunzi walio chafguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanakwenda kauanza masomo sehemu walizopangiwa.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika Hamadi Mapengo wakati akifunga kikao cha baraza la kawaida kilichofanyika ukumbi wa Mikutano halmashauri ya Tanganyika Mapengo amesema kuwa Madiwani wanao wajibu wa kuhamasisha na kusimamia wanafunzi walio faulu kujiunga na masomo yao kama walivyo pangiwa kwakuwa serikali imetengeneza miundo mbinu rafiki kwa wanafunzi hao.

‘’Niwaombe tu waheshimiwa  kipindi hiki mtu saidie sana Serikali watoto waliofaulu kwenda sekondari hatujawa na taarifa nzuri ya watoto kwenda shule au kulipoti sasa naomba twende tusaidiane kwa sababu ni sehemu ya majukumu yetu turudi  kwenye kata zetu tuhumize watendaji wa vijiji au sisi kanma kata tutafute takwimu na taarifa rasimi zinazoonesha kwakila siku kwamba watoto waliofaulu katika secondary zetu wangapi ambao wamelipoti nawangapi ambao hawajalipoti bahati nzuri tunazifahamu shule zile’’ amesema Mapengo.

Mapengo amewaomba Madiwani kuendelea kuibua Miradi ya kimukakati kwenye kulingana na mahitaji ya Kata zao kwa lengo la kuisadia serikali inapokuwa katika mipango ya kuleta huduma hizo kwenye kata zao.

Watumishi wa idara mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakiwa katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani
‘’Sisi madiwani tunajua vizuri kata zetu zinahitaji huduma gani kwa wakati huo tuwe wa kwanza kuwahamasisha wananchi kuibua miradi hiyo kwa vitendo”

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amesema halmashauri lazima kuendelea kubuni vyanzo vingi vya mapato na kusimamia vyanzo vilivyopo ili kuifanya halmashauri kuendelea kutekeleza miradi yake kwa ufasaha.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akitoa neno wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani Wilaya ya Tanganyika [Picha na Paul Mathias]

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya ameawaomba watendaji katika wilaya hiyo kuendelea kuwatumiakia wananchi kwa vitendo kwa kuwasaidia kutatua changamoto zao.

Akichangia hoja mbalimbali katika kikao hicho diwani wa Kata ya Tongwe Frank Kibigas ameshauri halmashauri kuendelea kupeleka Mashne za kukusanyia Mapato POS kwenye maeneo yanayo onekana kuwa na aina ya ukwepaji wa ushuru ili kuhakikisha maeneo hayo yanachangia halmashauri kwa kazi zinazofanyika.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages