VIJANA KATAVI TUCHAPE KAZI KWA BIDII


Mjumbe wa Baraza kuu la Taifa UVCCM Mkoa wa Katavi Mhandisi Debora Joseph akiwahutubia baraza la umoja wa vijana wilaya ya Tangantika mkoa wa Katavi[Picha na Paul Mathias]
Na paul Mathias- katavi.

Vijana katika mkoa wa katavi wameobwa kuwa waaminifu kwa kulejesha Mikopo ya fedha wanazo kopeshwa na halmashauri zao kupitia Asilimia nne kama maelekezo ya Serikali yanavyo elekeza.

Wajumbe wa Braza la umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi ccm Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wakiwa katika kikao cha Baraza hilo [Picha na Paul Mathias[
Vijana katika mkoa wa katavi wameobwa kuwa waaminifu kwa kulejesha Mikopo ya fedha wanazo kopeshwa na halmashauri zao kupitia Asilimia nne kama maelekezo ya Serikali yanavyo elekeza.

Hayo yameelezwa na Mjumbe wa Baraza kuu Taifa UVCCM Kutoka mkoa wa Katavi Mhandisi Debora Joseph wakati akihutubia kikao cha Baraza la umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tanganyika kilichofanyika katika Kijiji cha Majalila wilaya ya Tanganyika.

Debora amesema kuwa serikali imekuja na mpango wa kuwawezesha vijana mikopo kupitia halmashauri zao kwa asilimia nne ili kuwainua kiuchumi ila kumekuwa na Shida ya urejeshaji wa Mikopo hiyo kwenye halmashauri hali ambayo hupelekea wengine kukosa mikopo hiyo.

Mjumbe wa Baraza kuu Taifa UVCCM Kutoka mkoa wa Katavi Mhandisi Debora Joseph akizungumnza katika kikao cha baraza la umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tanganyika mapema leo[Picha na Paul Mathias]

‘’suala la mikopo limekuwa suala mtambuka linaumiza kichwa ukija huku upande wa serikali wanakuambia hivi ukija huku upande wetu wa chama tunaambiwa hivi sasa basi mimi nataka niseme hivi vijana wa ccm niwazembe nafasi tunazopewa tunaaminiwa tunazitumia vibaya ndio maana hatuaminiki mikopo tunapewa tunaaminiwa tunafika pale tumevaa kijani zetu tumependeza tunaheshimika haya sasa tumepewa mikopo tukafanye kazi tunapewa hiyo fursa kwenye kulejesha tunasema hali ni mbaya’’ amesema Debora.

Debora amesema kuwa kutokana na hali hiyo imewalazimu vinaja wengi kukosa fursa ya kupatiwa mikopo kutokana na vijana kukopa fedha hizo na kushidwa kuludisha hali inayopelekea vijana wengine kukosa fursa hiyo.

‘’twendeni sasa sisi ambao tupo sasa hivi tukailudishe ile Imani mtu ukipewa nafasi ndugu zangu tuitumie ile nafasi vizuri aliekupa nafasi asijute kukupa nafasi mikopo imekuwa na changamoto mikopo haturejeshi tunapoenda kuchukua ile mikopo tujilidhishe vijana wenzangu jambo unalotaka kwenda kufanya lipo sahihi litanilipa? ’’

Amesema sasa niwakati wa kuelezena ukweli kwa Vijana ili kutengeneza kiazazi cha Vijana chenye uchumi uliosimama bila kuteteleka kwa kufanya kazi kwa bidiii na nidhamu katika katika kazi za kila siku ili kuendelea kuaminika katika jamii.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi David Mussolin akipanda Mti katika shule ya Sekondari Majalila kabla ya mkutano wa baraza la wilaya la UVCCM Wilaya ya Tanganyika mkoa wa katavi[Picha na Paul mathias[
Amesema vijana ni nguzo ya chama cha Mapinduzi hivyo ni vyema kwenda kuyasema yale mazuri kwa wanachi yanayofanywa na Rais Dk Samia suluhu Hassan kwa wananchi kwa vitendo kupitia Miradi Mbalimbali ya Maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tanganyika David Mussolini katika wilaya ya Tanganyika vijiji tisa vimetenga maeneo ya kilimo kwa ajili ya vijana na mpaka sasa hivi kuna ekari Zaidi ya 200 zilizotengwa kwaajili ya kilimo kwa vijana.

‘’Kwa kata ya Mwese tunavijiji vine vijiji vitatu vimeanza kutenga maeneo,ukienda kijiji cha lugonesi tumebahatuka kutenga ekali 50 ambazo zipo na mimi kama mwenyekiti wa umoja wa vijana nimebahatika kwenda kuziona sambamba na hayo kijiji cha mwese kimeweza kutenga ekali 10 kwaajili ya vijana hapo mimi nimefika na kuziona na kijiji cha Lwega kimetenga Ekali 20 ambazo zipo’’

Mjumbe wa Baraza kuu Taifa UVCCM Kutoka Mkoa wa Katavi Mhandisi Debora Joseph akipanda Mti katika shule ya sekondari Majalila kabla ya kuhutuibia baraza la vijana la UVCCM Wilaya ya Tanganyika[ Picha na Paul Mathias]
Katika hatua nyingine David amebainisha kuwa wamekuwa wakiendelea kutoa hamasa ya vijana kuunda Vikundi ili kukopesheka kwa lengo la kujikwamua kiuchumi wao kama vijana.

Awali kabla ya kuanza kwa baraza hilo la umoja wa Vijana wa Wilaya ya Tanganyika Mjumbe wa Baraza kuu Taifa wa UVCCM Mkoa wa katatavi Mhandisi Debora Joseph ametembelea shule ya sekondari ya Majalila na kupanda miti pamoja na kutembelea Shule ya Sekondari Kakoso na Kujionea mwenendo wa Ujenzi wa Mradi wa Bweni shuleni hapo.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviblogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages