WATENDAJI WOTE WA KATA MLELE DC WAPATA PIKIPIKI ZA DKT SAMIA

 

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Mlele Teresia Irafay akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mlele Majidi Mwanga wakimkabidhi pikipiki Mtendaji wa kata Ilunde Jacksoni Shura
Na Paul Mthias,Mlele.

Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi imekabidhi pikipiki kwa watendaji wote wa Kata zilizopo katika Halmashauri hiyo zilizotolewa hivi karibuni na serikali ili kusaidia utendaji kazi kwa watendaji hao katika shughuli zao za kila siku.

Mhe. Majid Mwanga, Mkuu wa wilaya  Mlele akijaribia kuwasha pikipiki zilizotolewa na serikali kwa watendaji wa kata wakati wa  hafla ya kuwakabidhi iliyofanyika Halmashauri ya wilaya ya Mlele

Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi imekabidhi pikipiki kwa watendaji wote wa Kata zilizopo katika Halmashauri hiyo zilizotolewa hivi karibuni na serikali ili kusaidia utendaji kazi kwa watendaji hao katika shughuli zao za kila siku.

Akikabidhi pikipiki hizo katika Viunga vya ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri hiyo Teresia Irafay amewaasa watendaji hao kutumia pikipiki hizo kwa lengo lililokusudiwa ambalo ni kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

Irafay ameongeza kuwa pikipiki hizo ikawe chachu ya kufanya kazi kwa bidi na kuwafikia wanachi kwa wakati na kutatua changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kuhusu masuala mabalimbali ya kitaifa.

Wakati wa makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga ameshuhudia makabidhiano hayo yaliyoenda sambamba na watendaji hao kusaini Mkataba ya matumizi ya pikipiki hizo baina yao na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele.

Mhe. Majid  Mwanga mkuu wa wilaya ya Mlele katika waliokaa akiwa na mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Teresia Irafay wa kwanza kulia pamoja na watendaji wa Kata baada ya kuwakabidhi pikipiki hizo

Mkuu huyo wa Wilaya ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshiwa Dkt Samia Suluhu Hassan,kwa kuwajali watumishi wote na kuwapatia vitendea kazi ikiwemo magari, pikipiki na motisha mbalimbali ambazo zimekuwa ni chachu katika utendaji kazi kwa watumishi.

Nao baadhi ya Watendaji wa Kata waliopokea Pikipiki hizo wamesema kuwa watazitunza na kuzitumia kwa malengo yaliyo kusudiwa na wameishukuru serikali kwa kuwatatulia changamoto hiyo ya usafiri.

Abdala Saidi Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Mlele akitoa neno kwenye hafla hiyo amewaomba watendaji hao kuzingatia sheria za umiliki wa vyombo hivyo kwa kujifunza Zaidi katika taasisi zinazotoa mafunzo ya udereva na kupata Leseni ili waweze kutumia vyombo hivyo kwa mujibu wa sheria.

Serikali ya awamu ya Sita imekuwa ikiendelea kuboresha miundo mbinu ya watumishi hapa nchini kwa lengo la kuwasaidia kutimiza majukumu yao pasipo na kikwazo chochote.

Kwa habari zaidi Tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages