WASIO JULIKANA WAKATA NYAYA ZA TANESCO

 


Moja ya Trasfoma iliyopo Eneo la Mtemi Beda Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda iliyokatwa nyaya zake za shaba na watu wasiofahamika[Picha na Paul Mathias]
Na Paul Mathias -Katavi

Shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa katavi limesema halitamfumbia macho yeyote atakae bainika kuhujumu Miundo mbinu ya shirika hilo kwa kuharibu miundo mbinu kwa makusudi hali ambayo inayopelekea kukosekana kwa umeme kutokana na uharibifu huo.

Abeid Abeid Afisa usalama wa miundo mbinu ya Tanesco Mkoa wa katavi [katikati mwenye Koti]akiwa katika oparesheni maalumu ya kuangalia usalama wa miundo mbinu ya Tanesco Manispaa ya Mpanda [Picha na Paul Mathias] 

Shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa katavi limesema halitamfumbia macho yeyote atakae bainika kuhujumu Miundo mbinu ya shirika hilo kwa kuharibu miundo mbinu kwa makusudi hali ambayo inayopelekea kukosekana kwa umeme kutokana na uharibifu huo.

Rai hiyo imetolewa na Afisa usalama wa Miundo mbinu ya Tanesco Mkoa wa Katavi Abeid Abeid wakati  akiwa katika ukaguzi na uangalizi maalumu wa kujionea uharibifu wa miundo mbinu ya Transfoma kukatwa kwa Nyaya za Shaba zinazo zuia ladi kwenye baadhi ya Maeneo Manispaa ya Mpanda.

Amesema hadi sasa kuna maeneo Tisa ambayo  Trasnfoma zake zimehujumiwa kwa kukatawa nyaya hizo ikiwemo eneo la Mtaa wa Mtemi Beda kata ya Misunkumilo na eneo la Mtaa wa kapalangawe kata ya Kazima ambalo waharifu hao walishidwa kutekeleza uharifu huo kwa kukibizwa na wananchi wakati wa Mchana.

Ameeleza kuwa waharifu hao wamekuwa wakifanya vitendo hivyo vya kuhujumu miundombinu hiyo kwa kutumia vifaa kama Mapanga kukata nyaya hizo na kuzichukua na kuzipeleka kusiko julikana

Maafisa wa shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa Katavi wakiwa katika eneo la mtaa wa Mtemi Beda na kujionea uharibifu wa miundombinu ya Transfoma ilinyokatwa na watu wasio fahamika[Picha na Paul Mathias]

‘’tupo katika zoezi hili la kutokomeza uharifu unaofanywa na watu wasiojulikana kwa kushiriki kukata hizi nyanya na hili suala ni baya na halikubariki, kwanza ni hujuma sababu inaingizia hasala serikali sababu miundo mbinu hii inatumia gharama kubwa sana, kama mnavyoona katika eneo hili la kapalangao wanatumia vitu vye ncha kali kama mapanga kuhujumu miundo mbinu hii haikubaliki amesema Abeid’’

Amesema wale wote watakaobanika watakamatwa  na kuwafikisha katika vyombo vya sheria pasipokuwa na huruma dhidi yao

‘’na nisemetu walewote ambao tutawabaini na kuwakamata tutachukua hatua kali za kisheria na rai yangu kubwa nitoe wito  kwa wananchi walio karibu na maeneo haya wamepewa dhamana ya kulinda miundombinu kwa kutoa taarifa tanesco au kwa viongozi wao wa Mitaa’’amefafanua Abeid

Kwa upande wake Meneja wa Shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa katavi Seraphine Lyimo akizungumzia mikakati ya shirika hilo juu ya usalama wa miundo mbinu ya Tanesco mkoa wa Katavi amesema kuwa awali changamoto hiyo ililipotiwa katika maeneo ya Inyonga walifanya Doria na kufanikiwa kuwakamata na kuwa fikisha mahakamani.

Meneja wa shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa Katavi Mhandisi Seraphine Lyimo wakati akizungumza na mwandishi wa chombo hiki ofisini kwake [Picha na Paul Mathias]
Kwa siku za nyuma kwa Mpanda hatujawahi kupata tatizo la aina hii tuliwahi kupata shida hii eneo la Inyonga kule mlele ndipo walipokuwa wanakata nyaya kubwa lakini napo tuliitisha operesheni kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama wakakamatwa na kupelekwa Mahakamani na baada ya kupelekwa mahakamani tatizo hilo lilikwisha.

Lyimo amesema wimbi la waharifu hao lililoibuka kwa kukata nyaya za shaba kwenye baadhi ya maeneo ya Trasfoma za shirika hilo na wanaendelea kufanya dolia kwenye maeneo hayo ikiwamo hiyo waliyoianza kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kuwabaini waharifu hao.

Amefafanua kuwa wataendelea kutoa elimu kwa wanachi katika maeneo mbvalimbali ya mkoa wa Katavi juu ya umuhimu wa Kutunza miundombinu ya umeme kwenye maeneo yao kwakuwa serikali inawekeza fedha nyingi kujenga miundombinu ya umeme.

Nao baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Mtemi Beda ambapo Trasfoma ya imehujumiwa wameiomba serikali kupitia shirika la ume me Tanesco kuendelea kutoa elimu ikiwemo kuanzisha ulinzi shirikishi na jamii ya maeneo hayo ili kuzuia uhujumu huo unafanywa na baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema na maendeleo ya mkoa wa Katavi.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

Kataviblog.spot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages