WANAUME WASUSIA MAZISHI


Wanawake wa Kitongoji cha Namanyere Kata ya Majimoto Halmsahuri ya Mpimbwe mkoa wa Katavi wakichimba Kaburi baada ya wanaume wa Kitongoji hicho kugoma kushiriki zoezi hilo.
Na Paul Mathias

Wanaume wanaoishi katika Kitongoji cha Namanyere   Kata ya Maji Moto Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamesusia kufanya shughuli za mazishi ya watoto wanao fariki kwenye  Kitongoji hicho  wakidai idadi ya vifo vya watoto kuwa imekuwa kubwa  na badala yake  shughuli hiyo inafanywe na Wanawake .

Wanawake wa kitongoji cha namanyere wakiwa katika zoezi la Mazishi

Wanaume wanaoishi katika Kitongoji cha Namanyere   Kata ya Maji Moto Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamesusia kufanya shughuli za mazishi ya watoto wanao fariki kwenye Kitongoji hicho  wakidai idadi ya vifo vya watoto kuwa imekuwa kubwa  na badala yake  shughuli hiyo inafanywe na Wanawake  

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Namanyere  Teresiana  Wikula amesema hali hiyo imeleta mtafahaluko mkubwa  na mshituko katika historia ya wananchi wa Kitongoji hicho kwani haija wahi kutokea shughuli ya mazishi kufanywa na wanawake badala ya wanaume.

Mmoja wa wakazi wa Kijiji  hicho  John  Madirisha  amesema  kuwa wanaume wa Kitongoji hicho wamesusia kufanya shughuli za  mazishi  kutokana kuongezeka kwa idadi ya vifo vya watoto  wachanga hadi miaka miwili .

Amesema  idadi   hiyo ya vifo imekuwa   kubwa na kuanza kuwatia hofu  juu ya vifo hivyo na kuamini kuwa vifo hivyo vinatokana na nguvu ya giza .

‘’sisi tumechoka kuzika kila siku watoto wanakufa na hao wanaowaua ni baadhi ya wanawake wa kitongoji hiki kwa kisingizio cha Surua wazike wenyewe’’ amesema madirisha

Nae  Maiko Msanja  mkazi wa kitongoji hicho ameeleza kuwa idadi ya vifo  imekuwa ni kubwa kwenye  Kitongoji hicho kwani  idadi ya watoto wanao kufa kwa   wiki imefikia wan ne hadi watoto watano.

wanawake wa kitongoji cha Namanyere wakiwa katika mazishi 

Hivyo kutokana  na idadi kuwa kubwa  ya vifo vya watoto wao wanaume  wameona  wamechoka kufanya kufanya shughuli za mazishi na shughuli hiyo wamewaachia wanawake kwani wamekuwa wakijiuuliza kwanini vifo  vimekuwa vya mfululizo tena ni watoto tu.

Amesema kuwa  hapo nyuma kulikuwa na  mlipuko wa ugonjwa wa surua lakini hadi sasa bado vifo vimeendelea  kwa hari hiyo wao hawakubaliani vifo hivyo kutokana ugonjwa wa surua bali kuna  ushirikina  unao tokana na unaofanywa na baadhi ya wanawake kwenye Kitongoji hicho  kwa kisingizio cha ugonjwa wa surua  kwa hiyo na mazishi wafanye wanawake wenyewe wao wanaume wamechoka .

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Namanyere Kata ya Maji Moto  Teresia Wikula  amekiri kuwa  ni kweli wanaume wa Kitongoji hicho wamesusia kufanya shughuli za mazishi na shughuli hizo kwa sasa zinafanywa na wanawake.

Amebainisha kuwa  kwa wiki wamekuwa wakijikuta wanazika  watoto wane mpaka watoto watano hali ambayo haijawahi kutokea kenye kitongoji hicho.

Amesema mnamo  Desemba mwaka jana  kulilipuka ugonjwa wa surua  katika Kitongoji   hicho ambapo hadi sasa  bado kuna wimbi  la vifo kwenye Kitongoji  na yeye  haamini  kuwa vifo hivyo vinatokana na na imani za kishirikina ila anacho amini ni  mripuko wa ugonjwa wa surua.

Amesema  maafisa wa afya wamekuwa wakifika  Kitongojini hapo na  kuwa elimisha wananchi na kutowa chanjo lakini wananchi wamekuwa  na mwitikio mdogo.

Mwenyekiti huyo wa Kijiji ameomba wataalamu wa Afya  katika Halmashauri yao ya Mpimbwe waongeze nguvu  katika kukabiliana na ugonjwa huo ambao umechukuwa muda mrefu sasa.

Kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages