BABA HALISI NIWAJIBU WA KANISA KUWAOMBEA VIONGOZI WA NCHI YETU.

 

Baba halisi wa Kanisa halisi la Mungu Baba Tanzania akiongoza ibaada ya shukrani katika ukumbi wa Mpanda social hall Mpanda mjini.
Na Paul Mathias -Katavi.

Kanisa Halisi  la Mungu Baba Tanzania limesema kuwa litaendelea kuhimiza umoja na mshikamano kwa watanzania ili kuyafikia maendeleo ya kweli katika shughuli zao za kila siku

Mwakilishi wa mkuu wa Mkuu wa Katavi Kenneth Pesambili kulia akimbidhi Baba halisi stakabadhi ya malipo ya bank ya Shilingi milioni Tatu iliyotolewa na mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko kwa kanisa hilo.

Kanisa Halisi  la Mungu Baba Tanzania limesema kuwa litaendelea kuhimiza umoja na mshikamano kwa watanzania ili kuyafikia maendeleo ya kweli katika shughuli zao za kila siku

Hayo yameelezwa na Baba Halisi wa Kanisa Halisi la Mungu Baba wakati wa ibada ya shukurani kwa kulipokea kanisa iliyofanyika katika ukumbi wa Mpanda social hall Mpanda Mjini.

Mungu Baba amesema kanisa la halisi la Mungu Baba linawaombea watanzania wote pamoja na viongozi wa Taifa ili wafanikiwe kuliongoza taifa la Tanzania katika hali ya umoja mshikamano na upendo wenye Chemu chemu ya Baraka ya matumaini.


Amesema wameamua kufanya ibaada hiyo ya shukrani katika mkoa wa katavi kiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa kanisa hilo katika mkoa wa Katavi.

Katika ibaada hiyo ya shukurani mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Keneth Pesambili amesema kuwa mkoa wa katavi unatambua mchango wa viongozi wa dini katika mkoa wa katavi kwakuwa wanahubiri umoja na Amani kwa waumini wa mkoa wa katavi.

Pesa mbili amekabidhi skabadhi ya Bank ya shilingi Milioni 3 iliyotolewa na mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kwaajili ya kusaidia ujenzi wa kanisa hilo.

Kwa upande wake mtekelezaji wa sauti moja halisi kutoka Kanisa halisi  la Mungu Baba amesema kazi

 ‘’kubwa ya viongozi wa kanisa hilo nikufundisha maadili mema kwa jamii kama kanisa tunasisitiza mambo matatu kwanza Amani,upendo uliopitiliza,na uzalishaji wakati mungu Baba anamuumba Adamu alimpa bustani ya Aden ailime na kuitunza’’  

Amesema kuwa kila siku wamekuwa wakifanya Maombi kwaajili ya kuwaombea wanachi na Viongozi wa Taifa hili la Tanzania.

‘’kila siku sisi tunaanzaga ibaada saa kumi na moja Alfajiri  hadi saa kumi na mbili asubuhi vituo vyote Tanzania kwaajili ya kuombea watu wote serikali yote wanachi wote kwa nini Amani ikitokea basi upendo unatokea kwa watu wote’’

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages