Mwenyekiti wa chama cha kulinda na kutetea haki za walimu Tanzania Datus Mwakasanga akitoa neno la shukurani baada ya kuchaguliwa katika Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi . |
Chama cha Walimu cha kulinda na Kutetea
Haki za Walimu Tanzania (CHAKUHAWATA)
kIlichoanzishwa hivi karibuni katika Manispaa ya Mpanda
kimepata viongozi wake wapya watao kiongoza chama hicho kuhu kikiwa kimepata
idadi kubwa ya wanachama waliokuwa wanachama wa chama cha walimu CWT .
Wajumbe wa chama cha kulinda na kutetea haki za walimu manispaa ya Mpanda wakiwa katika uchaguzi wa viongozi wao |
Kati ya idadi ya walimu 891 waliopo katika shule
za Msingi na Sekondari CHAKUHAWATA kimeweza kufanikiwa kwa kipindi
hiki kifupi kuwa na idadi ya wanachama 632 ambao ni sawa na asilimia 90 ya
walimu wote waliopo katika Manispaa ya Mpanda .
Viongozi wa chama hicho waliochaguliwa kwenye mkutano mkuu wa Chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Mpanda nafasi ya Mwenyekiti wa Chama cha CHAKUHAWATA Wilaya ya Mpanda ni Datus Mwakasanga alipata kura 26 dhidi ya Benjamini Masai aliyepata kura 25 ,katibu amechaguliwa kuwa ni Nyavidunda Mhule .
Benjamini Masai Mgombea akiomba kura kwa wajumbe kwa unyenyekevu lakini katika uchaguzi huo kura hazikutosha za kuwa mwenyekiti wa chama hicho. |
Akisoma taarifa ya chama hicho kabla ya kuanza kwa uchaguzi aliyekuwa kaimu Katibu Chakuhawata Nyavidunda Mhule Wilaya ya Mpanda alisema kuwa chama hicho katika Wilaya ya Mpanda kilianza mwaka 2021 kikiwa na mwanachama mmoja hadi sasa kina wanachama 632 kati ya wanachama 891 walipo katika Manispaa ya Mpanda .
Amebainisha kuwa chama hicho kimekuwa na mafanikio
ikiwa ni pamoja na kongeza wanachama kwa idadi kubwa ,kutowa elimu kwa
wanachama kuhusu uwajibikaji kutowa namna bora juu ya kudai haki .
Safu ya uongozi Mpya wa Chama cha Kulinda na kutetea Haki za Tanzania Katika manispaa ya Mpanda baada ya kuchaguliwa. |
Katibu msaidizi tume ya utumishi wa
walimu amesema viongozi wasifurahie kuchaguliwa bali
wahakikishe wanaisaidia tume ya utumishi wa walimukutatua migogoro
ya walimu na pia watowe huduma bora kwa wanachama wao .
Amewaonya kutojihusisha na malumbano na chama kingine cha
Walimu cha CWT na badala yake wanatakiwa
kuhakikisha wanafanya kazi ya kukijenga chama chao kwa masilahi mapana ya
wanachama wao
Kwa upande wake mdhibiti wa ubora elimu wa Manispaa ya
Mpanda Leonald Simbeye amesema kuwa chama hicho
kinatakiwa kufanya kazi zake kwa kuzingatia katiba yao na si kufanya kazi
za kupingana na Serikali.