KAMATI ZA PETS NSIMBO JICHO LA WANANCHI MIRADI YA SERIKALI

Mratibu wa Mradi wa PETS kutoka shirika la Grean Leaf akitoa taarifa ya mwenendo wa mradi katika halmashauri ya Nsimbo.
Na Paul Mathias -Nsimbo 

Shirika la Grean Leaf Tanzania inayotekeleza Mradi wa kuwajengea uwezo wananchi kuhusu ufatiliaji wa matumizi ya fedha za umma katika miradi ya elimu ya Msingi  Katika halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi imesema wananchi wamekuwa na uelewa juu ya Ushilikishwaji na ushiriki wa jamii wa matumizi ya fedha za umma zinazoletwa na Serikali .

Wajumbe wa Kamati za Pets walio chuchumaa wakiwa na kaimu mkurugenzi Halmashauri ya Nsimbo Erimkwasi Jonh pamoja na madiwani na Mratibu wa Mradi wa Pets wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa kikao cha kupata mrejesho kutoka kamati za Pets.

Shirika la Grean Leaf Tanzania inayotekeleza Mradi wa kuwajengea uwezo wananchi kuhusu ufatiliaji wa matumizi ya fedha za umma katika miradi ya elimu ya Msingi  Katika halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi imesema wananchi wamekuwa na uelewa juu ya Ushilikishwaji na ushiriki wa jamii wa matumizi ya fedha za umma zinazoletwa na Serikali .

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa huo mradi Anord Lumbi wakati wa kikao cha Mrejesho kamati za PETS Katika maeneo ya Mradi unapotekelezwa katika kata za Kanoge,Katumba,Kapalala na Nsimbo.

Anord amebainisha kuwa Mradi huo unatekelezwa na Taasisi ya Green Leaf Organization kwa ufadhili wa Shirika la Foundation for civil society wenye Gharama ya shilingi million 39 ambapo jumla ya shule nane za msingi katika kata hizo zitanufaika na mradi huo.

Joyce Benedictor Mwenyekiti wa Kamati ya Pets akitoa taarifa ya Mrejesho kwa kazi iliyofanywa na kamati hiyo katika maeneo ya mradi wa Pets katika kata nne za Halmashauri ya Nsimbo.

Amesema kamati za ufatitiliaji katika kata zimeshapatiwa mafunzo ya uelewa juu ya Ufatiliaji wa Fedha za serikali zinazoletwa katikia miradi ya maendeleo na tayari kamati hizo zimeanza kufanya kazi ya tathimini na uelewa kwa wananchi kuhusu fedha za miaradi zinazo letwa na serikali.

Awali akiwasilisha taarifa ya Mrejesho wa [PETS] kwa kata zinazonufaika na mradi huo Joyce Benedictor amebainisha kuwa kamati hizo zimebaini baadhi ya changamoto ikiwemo Mrundikano wa Wanafunzi kwa baadhi ya shule,Miundombinu kutokuwa toshelevu,Uchakavu kwa baadhi ya Majengo ya shule  pamoja na Rasilimali watu kuwa chache kwenye baadhi ya shule.

Ameishauri serikali kuendelea kuzitatua kero hizo kwa kadri inavyowezekana ili kuhakikisha watoto wanapata elimu katika mazingira salama.

Katika hatua nyingine ameipongeza serikali kwa kuendelea kutatua changamoto ya miundombinu kwa ujenzi wa Madarasa na Mabweni kwa wanafunzi.

Baadhi ya Madiwani walioshiriki katika kikao cha Mrejesho wa kamati za Pets wakiwa na kaimu mkurugenzi Halmashauri ya Nsimbo Erimkwasi Jonh[ wa Tatu toka kushoto]

Kaimu mkurugenzi Halmsahauri ya Nsimbo Erimkwasi Jonh amesema kuwa Mradi wa PETS Tangu aauanze kutekelezwa umekuwa na manufaa kwa wananchi na halmshauri kwa kuwaongezea uelewa watendaji wa serikali na wananchi juu ya kutimiza wajibu wao na uwajibikaji kwenye shule zao.

‘’wananchi kupitia kamati hizi za PETS wananchi wameamka wameweza kufatilia matumizi ya fedha za umma katika shule zetu hizi kwa ukaribu sana imewafanya hata waalimu katika shughuli zinazo husu fedha kuziweka wazi katika mbao za matangazo amesema Erimkwasi’’

Amebainisha kazi mbalimbali zinazo husu ujenzi kwa kuwapata mafundi umekuwa shirikishi kwa kufuata kanuni na taratibu kwa uwazi zaidi hii inatokana na kamati hizi za PETS kusimamia uwajibikaji.

Diwani wa Kata ya Katumba Rajab Said akizumgumzia namna Mradi wa Pets unavyotekelezwa katika kata ya Katumba.

Pamoja na hayo ameeleza kuwa serikali ya wamu ya Sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan imekuwa ikiendelea kuleta fedha katika halmashauri ya Nsimbo kwaajili ya kuboresha miundombinu ya shule hivi karibuni halmashauri hiyo imepokea kiasi cha Shilingi Bilion 1.8   kupitia Mradi wa BUST kwaajili ya kwenda kujenga shule mpya mbili zinazojitosheleza kwa miundombinu zote.

Diwani wa kata ya Kanoge Salehe Mrisho na diwani wa Kata ya Katumba Rajabu Said wamebainisha kuwa Grean Leaf kupitia Mradi wa PETS umeawasadia madiwani kuweza kufatilia kwa kina matumizi ya fedha zinazoletwa na serikali kwenye kata zao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages