WAFANYA BIASHARA SOKO LA MITUMBA WAIPA TANO HALMASHAURI YA MANISPAA YA MPANDA

Moja ya bidhaa zinazopatikana katika soko la Mitumba eneo la Kituo cha zamani cha Mabasi maalufu Stand ya zamani Mpanda Mjini

Na Paul mathias Katavi.

Wafanyabiashara wa Mitumba Eneo la Stand ya Zamani Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wameiomba serikali kuendelea kuboresha Miundo mbinu ya soko hilo ikiwemo Maji,Taa.

Baadhi ya wafanya biashara katika soko la mitumba eneo la stand ya zamani wakiwa katika kazi zao za kila siku.

Wafanyabiashara wa Mitumba Eneo la Stand ya Zamani Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wameiomba serikali kuendelea kuboresha Miundo mbinu ya soko hilo ikiwemo Maji,Taa ,na kumwaga Vifusi kwenye maeneo yanayoonekana kuwa na Mabonde mabonde.

Wakizungumnza kwa nyakati tofauti wakiwa sokoni hapo na Chombo hiki wamesema  kuwa kutokana na hali ya sasa Sokoni hapo Mfumo wa maji uliopo ni maalumu kwaajili ya huduma ya vyooni na si kwaajili ya matumizi mengine ya maji sokoni hapo.

Wamebainisha kuwa hali hiyo imekuwa ikiwapa shida na kuingia gharama ya kununua maji shilingi 250 kwa dumu moja kwaajili ya matumizi mengine ya kawaida sokoni hapo.

‘’Inatulazimu kununua maji kwa sababu yaliyopo nikwaajili ya huduma ya choo hali ambayo kiafya huwezi kuyatumia ikizingatiwa Tank la Maji lipo Karibu na Choo ‘’amesema mmoja wa wafanyabiashara hao sokoni hapo.

Wamesema kutokana na Shughuli kuendelea kufanyika hadi nyakati za usiku wanaomba mamlaka zinazo husika kuwafungia Taa za kisasa ili kuendelea kufanya kazi zao  hadi  nyakati za usiku tofauti na sasa ambapo huwalazimu kufunga Mapema.

Katika hatua nyingine wameishukuru halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kufanya maamuzi ya kuziruhusu Gari ziendazo Vijijini Kuegesha hapo hali ambayo imeongeza mara dufu wateja wa biashara zao husususani Nguo,Vyakula na usafiri wa Boda boda kupata wateja.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli akizungumzia mikakati ya kuendelea kuboresha miundo mbinu ya soko la mitumba Stand ya zamani.

Peter Salvatory ‘’anasema zamani sisi Boba boda hapa ilikuwa mtihani kupata Abiria kwa siku ilikuwa kama bahati ila kwa sasa ujio wa Magari haya tunaishukuru halmashauri’’

Maria Jonh Mamalishe katika soko hilo amesema ‘’mimi nimekuwa hapa kwa muda mrefu zamani tulikuwa tunalaza vyakula kwa kukosa wateja ila leo tunashukuru baada ya Magari haya kutoka vijijijini kuruhusiwa kufanya maegesho hapa tunapata wateja’’

Mwenyekiti wa Soko hilo Jofley Tendesigulu ameishukuru halmashauri kwa kuona umuhimu wa kuipa uhai Stand ya Zamani kwa Magari ya vijijini kuegesha katika eneo hilo hali ambayo imeongeza wateja katika Biashara zao.

Moja ya mama lishe katika eneo la stand ya zamani akiwa katika kazi zake 

Amesema changamoto wanayoipitia ni Maji kwaajili ya Matumizi ya kawaida sikoni hapo na Tayari wamesha andika Barua kwa Mkurugenzi kuwaomba Muwasa kufunga Gati kwaajili ya kuwapatia maji kwenye matumizi mengine.

‘’tunamia Maji ambayo yanatoka maeneo ya chooni kule kuna bomba ambalolinafunguliwa kwenye eneo la choo ingawa wengi hawatumiii katika matumizi ya kawaida na tayari tumeandika barua kwa mkurugenzi wa Manispaa ya kuwaomba Muwasa watufungie Gati kwaajili ya matumizi memngine ya Maji sokoni hapo ‘

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages