CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU KATAVI CHA SHAULIWA KUSHIRIKISHA WADAU KUKUZA SOKA.

 

Mgeni rasmi Idd Kimata,Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi akizungumza wakati wa mkutano mkuu wa 2022 wa chama cha  mpira wa miguu  Mkoa wa Katavi uliofaanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Mansipaa ya Mpanda.

Walter Mguluchuma na Paul Mathias Katavi.

Chama cha  Mpira wa  Miguu  Mkoa wa Katavi (KRFA) kimeshaurikushirikisha wadau mbambali wa michezo  waliko  mkoani hapa nan je ya Mkoa  ikiwa ni katika jitihada za  kuinua soka la Mkoa huu na kuendeleza  vipaji kwa  vijana.

Chama cha  Mpira wa  Miguu  Mkoa wa Katavi (KRFA)  kimeshaurikushirikisha wadau mbambali wa michezo  waliko  mkoani hapa nan je ya Mkoa  ikiwa ni katika jitihada za  kuinua soka la Mkoa huu na kuendeleza  vipaji kwa  vijana .

Ushauri huu umetolewa  katika ufunguzi wa   Mkutano  mkuu wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya  Mpanda  na mgeni rasmi wa mkutano  huo Mwenyekiti wa  Chama cha  Mapinduzi Mkoa wa Katavi  Idd  Hassan  Kimanta( Mkuu wa Mkoa Mstaafu) kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano .

Amesema kuwa  mkoa wa Katavi kuna vipaji vikubwa sana vya vijana wanao jua kucheza mpira isipokuwa bado hawaja  shirikishwa inavyotakiwa kwa kuwakusanya vijana wa kutoka maeneo mbambambali kama  vile ya mwambao mwa ziwa Tanganyia na kuwaandalia mashindano mbambambali ya kuanzia ngazi ya Kata na kuendelea.

Kimanta ameshauri kuwa ili kuweza kuendeleza soka kwa Mkoa wa Katavi ni lazima  KRFA  iwashirikishe wadau mbali mbali wa soka wa   ndani ya Mkoa huu na wale wan je ya Mkoa wa Katavi

Amesema kuwa watu wacheze mpira  wasishindwe kucheza mpira kwa kisingizio  cha viwanja kwani viwanja vipo watumie hata  viwanja vya shule za msingi pindi wanafunzi watakapo kuwa  wametoka shuleni .

Amebainisha kuwa hakuna kitu kigumu kama kuendesha timu kwa sababu wachezaji wanapaswa kutuzwa sasa unawatunzaje pia wanahitaji vifaa vya mpira  mfano mpira mmoja mzuri ni laki mbili na nusu  hivyo bila kuwa na wadau timu haiwezi kuumudu gharama ya kuendesha timu .

Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Katavi Keneth Pesambili amesema chama hicho kinapata changamoto  kubwa ya timu inapokuwa imepata nafasi ya kuwakilisha  Mkoa kwenye mashindano kama ya mabingwa  wa  mikoa jukumu hilo la timu limekuwa ni kama la chama cha soka cha mpira wa miguu  Mkoa wa Katavi  hiyo ni kutokana na  vilabu husika kutokuwa na  ufadhili ..

Amesema kama timu zitapata udhamini  kuna uhakika wa timu za kutoka Mkoa wa Katavi  zikawa zinafanya vizuri kama ambavyo ilivyokuwa  timu ya Katavi Renger iliyokuwa  ikimilikiwa na Halmashauri.

Amevitaka vyama vya  mpira wa miguu vya kwenye Wilaya hiyo kuhakikisha ligi ya ngazi ya Wilaya inachezwa kwenye kila Wilaya ili mpira uchezwe kwenye maeneo yote kuliko ilivyo sasa ambapo kuna Wilaya zimekuwa hazifanyi mashindano ya ligi kwenye ngazi zao .

 Pesembili amewaambia wajumbe wa mkutano huo mkuu wa KRFA kuwa wao wamekuwa wakihakisha kila mwaka wanafanya mashindano yote ya kuanzia mashindano ya vijana  na mashindano mengine yote ambayo yapo kwa mujibu  TFF.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages