MBUNGE TUSKER MBOGO AIKUMBUKA UWT KATAVI.

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi,Tusker Mbogo akizungumnza wakati wa kukabidhi Pikipiki nne kwa Jumuiya ya wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi.
Na Paul Mathias- Katavi

Mbunge wa Viti Maalumu katika mkoa wa Katavi Tusker Mbogo ametoa Pikipiki nne Zenye zaidi ya Milioni 10 kwa Jumuiya Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM  Mkoa wa Katavi kwa lengo la kujiimalisha kiuchumi.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa katavi Iddi Kimanta akipokea vielelezo vya Pikipiki kutoka Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa katavi Tusker Mbogo.

Mbunge wa Viti Maalumu katika mkoa wa Katavi Tusker Mbogo ametoa Pikipiki nne Zenye zaidi ya Milion 10 kwa Jumuiya Umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM  Mkoa wa Katavi kwa lengo la kujiimalisha kiuchumi.

Ajkizungumnza katika hafla ya kukabidhi Pikipiki hizo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano katika Ofisi za Chama cha Mpainduzi Wilaya ya Mpanda mbele ya Mgeni Rasimi katika shuhguli hiyo Mwenyekiti wa chama cha Mpanduzi Mkoa wa Katavi Iddy Kimanta.

Tusker amesema kuwa kwa kutambua mchango unaotolewa na Jumuiya ya umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi CC Mkoa wa Katavi UWT amewiwa kutoa pikipiki hizo ili zisaidie katika kuimalisha uchumi wa jumuiya hiyo ndani ya chama cha mapinduzi mkoa wa Katavi.

‘’Nimeona ni wajibu wangu kama mbunge wa viti maalumu wa mkoa wa Katavi kutoa pikipiki hizi ambazo zitakuwa kama mradi wa bodaboda ili uweze kuiendeleza jumuiya ya UWT na akina mama wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Katavi amesema “Tusker

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi Fortunatus Kabeja wa[ kwanza kulia] akiwa na mwenye kiti wa CCM mkoa wa Katavi Iddi Kimanta wakimkabidhi zawadi Mbunge wa Viti Maalumu Tusker Mbogo.

Amebainisha kuwa katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ili kukabiliana na changamoto ya kushidwa kuyafikia badhi ya maeneo katika kunadi sera za chama cha mapinduzi vyombo hivyo vya usafiri vitasaidia kwa namna moja au nyingine kuhakikisha wanawake wa chama cha mnapinduzi kupitia UWT wanawafikia wanachama na wapigakura kwa ulahisi zaidi.

“Lakini pia tunapokwenda kwenye uchaguzi w serikali za mitaa iliiakina mama hawa waweze kufanya kampeni Vizuri lakini tunapo kwenda katika uchaguzi wa 2025 wasije kusema tumekosa usafiri katika utekelezaji wa majukumu yao katika nyakati hizo za uchaguzi”

Kuhusu kazi zinazofanywa na serikali ya awamu ya Sita Chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan Tusker Mbogo amesema kumeshuhudiwa maendeleo katika sekta za Barabara,Maji,Afya,Elimu pamoja na mageuzi mbalimbali katika sekta za nishati na uwekezaji katika mkoa wa Katavi tofauti na miaka mingi ilivyokuwa.

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi Iddy Kimanta amesema msingi wa chama cha mapinduzi ni kusimamia Vitega uchumi vilivyopo ndani ya chama cha mapinduzi mkoa wa Katavi na hatomuonea mtu ambaye anahujumu kulipa mapato yanayotokana na vyanzo mapato ndani ya chama hususani Vibanda.

Baadhi ya wanawake wa UWT mkoa wa katavi wakiwa katika hafla ya kukabidhiwa pikipiki
“nitoe rai kwa wale wote ambao wamepanga vibanda vinavyomilikiwa na chama cha Mapinduzi walipe wakilipa wanakijenga chama cha Mapinduzi kiuchumi nazani kuanzia wiki ijayo tutanza kufatilia tusije tukalaumina katika suala la kukijengea chama cha Mapinduzi kwa nguvu za kiuchumi “amesema Kimanta

Katika hatua nnyingine amemshukuru Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Katavi kwa kutoa pikipiki hizo ambazo zitaisadia jumuiya ya UWT Kujiendesha kichumi hali itayosaidia chama cha mapinduzi kuendelea kuwaimala zaidi.

Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Katavi Fortunatus Kabeja awali akitoa salamu kwa niaba ya jumuiya hiyo amesema jamii lazima iendelee kuwalea watoto katika misingi ya maadili ya kitanzania na kuepuka tabia za kufuata mikumbo na kuiga tamaduni za kigeni.

wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa katavi wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho Iddi Kimanta katika 

Sisi kama wanawake tukatae ukatili wa kijinsia kwa watoto wetu na tuwalee katika maadili na misingi ya kitanzania ili kuendelea kuwa kizazi chenye maadili kwenye jamii”

Pikipiki hizo zilizotolewa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi Tusker Mbogo zimeakabidhiwa kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi na kugawiwa kwa Makatibu wa UWT katika wilaya za Mpanda, Mlele, Tanganyika, Huku chama cha Mapinduzi CCM  mkoa kikipatiwa pikipiki moja.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages