RC: MRINDOKO "TUNAJIVUNIA UWEPO WA SEKTA YA MADINI"

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumnza na viongozi mbalimbali wa Mgodi wa Katavi Mining katika ziara yake ya kutembelea maeneo yanayofanya shughuli za uchimbaji wa Madini katika mkoa wa Katavi.

Na Paul mathias-Katavi

Serikali katika mkoa wa Katavi imesema inatambua mchango unaotolewa na sekta ya madini kwa kuchangia pato la serikali na kukuza uchumi wa mkoa wa Katavi.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko [wanne kutoka kulia] akiwa katika ziara ya kutembelea maeneo ya uchimbaji wa madini katika mgodi wa madini wa Katavi Mining.
Akiwa katika ziara ya kutembelea wawekezaji wa Uchimbaji wa Madini katika mkoa wa Katavi ,Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema moja ya sekta muhimu inayochangia pakubwa katika ukusaji wa mapato ya serikali ni sekta ya Madini.

‘’tulipoanza soko hili mwaka 2019 dhahabu ambayo ilikuwa inauzwa wakati huo ilikuwa ni 801 .5 Gram ambazo thamani yake ni kama Milioni 62 lakini mpaka sasa tunavyozungumnza tulipo hapa march 2023 tayari kwa kutumia soko hili mkoa umeweza kukusanya dhahabu Tani 1.185 kwa maana ya kilo milioni moja lakimoja na semanini na tano elf mia saba semanini na sita  zenye thamani ya Bilioni 130.1 hayo ni mafanikio makubwa katika sekta ya madini’’amesema mrindoko

Akiwa katika soko hilo la madini mkoa wa Katavi Mrindoko amesema serikali itaendelea kuimalisha miundombinu katika sekta ya madini ili serikali iendelee kupata mapato kupitia madini.

Mohamed Abdullazak Mwekezaji wa Mgodi wa Katavi Mining [wa kwanza kulia] akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Mrindoko baada ya kutembelea mgodi huo.

Afisa madini Mkoa wa Ktavi Andrew Mwalugaja amesema kuwa kumekuwa na ongezeko la uzalishaji wa madini kukichagizwa na uwepo wa soko la madini katika mkoa wa Katavi hali ambayo imechochea ukuaji wa kiuchumi kupitia mapato ya madini.

Twaribu Serf Meneja wa Katavi Mining amesema changamoto ya uendeshaji wa Mgodi huo kwa kutegemea umeme wa mafuta umekuwa ukiwa gharimu na kuiomba serikali pindi umeme wa Grid ya Taifa ya umeme utakapo fika katika mkoa wa Katavi Mgodi huo upewa kipaombele ili kupunguza gharama za uendeshaji kwa kutegemea umeme wamafuta ya Disel.

Sehemu ya mitambo inayotumika katika shughuli mbambali kwenye Mgodi wa Madini wa katavi Mining.
Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa wa Katavi ametembelea Soko la Madini Mkoa wa Katavi,Mgodi wa Madini wa Katavi Mining na Mgodi wa Madini wa JIUXING TANZANIA MINING COMPANY LIMITED lengo likiwa nikujionea namna sekta ya madini katika mkoa wa Katavi inavyo fanya kazi na mchango wake katika ukuzaji wa uchumi wa mkoa wa Katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages