KATAVI YAJIPANGA KUKABILIANA NA UPUNGUFU WA MADARASA.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akihutunia wajumbe wa kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa (RCC) katika ukumbi wa Mikutona wa manispaa ya Mpanda iliyofanyika hivi karibuni-(Na picha na George Mwigulu)

Na   Walter Mguluchuma, Katavi.

Mkoa wa Katavi  katika   kukabiliana na tatizo la  upungufu wa vyumba vya madarasa katika Mkoa huu wamepanga  kujenga     maboma ya madarasa 500 ili kukabiliana na tatizo la upungufu  katika shule za Msingi katika Mkoa huu kutokana na kasi kubwa  ya sasa ya watoto kujiunga na masomo ya shule za Msingi.

Mkoa wa Katavi  katika   kukabiliana na tatizo la  upungufu wa vyumba vya madarasa katika Mkoa huu wamepanga  kujenga     maboma ya madarasa 500 ili kukabiliana na tatizo la upungufu  katika shule za Msingi katika Mkoa huu kutokana na kasi kubwa  ya sasa ya watoto kujiunga na masomo ya shule za Msingi.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa  Katavi Mwanamvua Mrindoko wakati alipokuwa akiwatubia wajumbe wa kikao 20 wa  kamati ya ushauri ya Mkoa wa Katavi (RCC) kilichofanyika  katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.

Mrindoko amebainisha kuwa  kwakutambua  hali hiyo  Mkoa wa Katavi  umejiwekea mkakati wa kuondoa kabisa tatizo la upungufu wa    vyumba vya madarasa kwa  kuwa na mkakati endelevu  na kuweka malengo  mbambali  mbali kwenye kila Halmashauri ya Mkoa huu.

Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kamati ya RCC Wakiwa kwenye ukumbi wa manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi .

Ametaja mikakati hiyo ni kila Halmashauri  wamekubaliana kujenga  vyumba  vya  madarasa   mia moja kwa kila Halmashauri ya  iliyopo kwenye Halmashauri  iliyo kwenye Mkoa  huu.

Mrindoko amefafanua kuwa kutokana na Mkoa  kuwa na Halmashauri    tano na kila Halmashauri kwenye mapato yake ya ndani   kwa mwaka wa fedha zimetenga  kujenga majengo  ya mabomamia moja hivyo kwa mkoa mzima wanatarajia kujenga  maboma 500 ya madarasa .

Amesema kuwa Mkoa wameisha  wasiliana na TAMISEMI ambao wamekubali kutuma pesa ya maboma yote kwa ajiri ya kukamilisha ujenzi  wa madarasa hayo pindi maboma hayo yatakapokuwa  tayari .

Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidari Sumry   amesema kuwa  Manispaa ya Mpanda  watahakikisha  wanatimiza ujenzi wa  madoma ya madarasa waliyopanga kuyajenga kwa mapato yao ya ndani .

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo amewahakikishia wajumbe wa kikao hicho kuwa swala hilo la ujenzi wa  maboma kwenye Halmashauri litatekelezwa kama ilivyopangwa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages