Meneja wa TANROADS Mkoa wa Katavi Mhandisi Martini Mwakabende akiwasilisha Rasimu ya Bajeti ya Tanroads Mkoa wa Katavi kwa Mwaka 2023/2024[Picha na Paul Mathias] |
Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Katavi imepanga kutumia kiasi cha Zaidi ya Tshs Bilioni 21 kwaajiri ya matengenezo ya barabara kwa ajiri yam waka wa fedha 2023/2024 huku Zaidi ya Tshs Bilioni 10 zikiwa ni kutoka mfuko wa Barabara.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akifungua kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika leo katika ukumbi wa manispaa ya Mpanda.- (Na picha na Paul Mathias) |
Hayo
yamesemwa na Meneja wa Taroads Mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende
wakati alipokuwa akiwasilisha rasimu ya bajeti ya Taroads Mkoa wa Katavi yam
waka wa fedha 2023/2024 kwenye kikao cha 20 cha
Bodi ya barabara ya Barara ya Mkoa wa Katavi kilichofanyika
katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda .
Mwakabende
ameeleza kuwa kwa mwaka ujao wa fedha wameomba kuizinishiwa bajeti
ya kiasi cha Tshs Bilioni 21. 885 kati ya fedha hizo Tshs
10,581,392 fedha za kutoka mfuko wa barabara na kiasi cha
Tshs Bilioni 11, 304,600,000 ni za kutoka mfuko wa Maendeleo .
Amesema
katika mwaka wa fedha 2022/2023 walitengewa kiasi cha Tshs Bilioni 17.2
kwa ajiri ya kufanyia matengenezo barabara na ukarabati na
hadi kufikia tarehe 28/2/ 2023 walikuwa wamepokea kiasi cha
Tshs Bilioni 7.1 ambazo ni sawa na asilimia 55. 98 ya bajeti ya
matengenezo ya barabara
Amebainisha kuwa TANROADS Mkoa wa Katavi wameendelea kuthibiti magari mazito kwa kuyapima na mizigo na yakibainika yamezidisha uzito hutozwa gharama za uharibifu kwa mujibu wa sheria ya usalama Barabarani yam waka ( Road Trafffic Act) 1973 kwa lengo la kutunza usalama na kudhibiti uzito wa magari barabarani .
Mwakabende amezitaja changamoto zilizopo kwenye utekelezaji wa kazi zao kuwa ni wananchi kupitisha mifugo yao barabarani na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa barabara , wananchi kufanya shughuli za kilimo ndani ya maeneo ya Hifadhi ya Barabara kama ya Kagwila kwenda Karema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Ali Makame Hamadi akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Katavi[Picha na Paul Mathias] |
Pia fedha zinazotolewa kwa ajiri ya miradi ya maendeleo kutokidhi mahitaji halisi ya ukarabati wa barabara na uharibifu wa alama za usalama barabarani kunaongeza gharama za matengenezo ya barabara na kuhatarisha usalama wa watumiaji wa barabara.
Mbunge
wa Jimbo la Mpanda Sebastian Kapufi aliomba Taroads
kuwalipa haraka wananchi fidia zao waliopisha ujenzi wa barabara za Mpanda
Sitalike na Mpanda Ugalla ambao wanamuda mrefu sasa hawaja lipwa
fidia zao .
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Sudi Mbogo amewapongeza Taroads Mkoa wa
Katavi kwa kazi nzuri wanayofanya ya ujenzi wa barabara na kuzisimamia
vizuri hali ambayo imefanya ulahisishaji wa usafiri .
Mkuu wa
Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko alisema ni kweli kuna changamoto ya
watu kuharibu miundo mbinu ya barabara hivyo ameliagiza jeshi la polisi
kuwasaka na kuwakamata watu wote wanaofanya uharibifu huo na kwa wale watao
bainika kununua miundo mbinu hiyo kama vyuma chakavu hata sita mara moja
kuwachukulia hatua .
Ameshauri
elimu ya utunzaji wa barabara kwa wananchi iendelee kutolewa kwani
ni muhimu wananchi kuelewa umuhimu wa barabara zinapo kuwa zinapita
kwenye maeneo yao .
Rc
Mrindoko kuhusu fidia za wananchi wanao dai amesema kuwa Serikali kweli
inatambua kuwa wananchi hao wanadai fidia na ipo katika hatua mbambali
juu ya utekelezaji wa swala hilo .