MBUNGE AWALILIA WANANCHI WALIOPISHA UJENZI WA BARABARA.


Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Mkoa wa Katavi,Sebastian Kapufi akichangia hoja zilizoibuka kwenye kikao  cha bodi ya barabara Mkoa wa Katavi- (Na Picha na George Mwigulu)

Na Walter Mguluchuma, Katavi

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini ameomba wananchi waliopisha ujenzi wa Barabara za kiwango cha lami  za  Mpanda   Sitalike na  Kawajense  kwenda Ugalla walipwe fidia zao wanazodai kwa muda mrefu sasa.

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Katavi,Mhadisi Martin Mwakabende akitoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali ya barabara kwenye kikao cha bodi ya barabara mkoa wa Katavi- (Na Picha Paul Mathias)

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini ameomba wananchi waliopisha ujenzi wa Barabara za kiwango cha lami  za  Mpanda   Sitalike na  Kawajense  kwenda Ugalla walipwe fidia zao wanazodai kwa muda mrefu sasa .

Kapufi ametowa kilio cha wananchi hao wakati wa kikao cha bodi ya barabara cha Mkoa wa Katavi  kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri  ya Manispaa ya Mpanda kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa  Katavi Mwanamvua Mrindoko .

Amebainisha kuwa kuna  wananchi wamepisha ujenzi wa barabara za kiwango cha Lami kutoka Mpanda kwenda Sitalike na Kawajense kwenda Ugalla wanadai fedha zao kwa muda mrefu sasa  nab ado hawaja lipwa fidia zao hizo .

Amesema hali hiyo inawafanya wananchi waliopisha ujenzi huo kuanguka kiuchumi kwani nyumba zao zimepigwa alama ya x ambayo inaamanisha kuwa wanatakiwa  walipwe fidia zao  kama ambavyo walivyofanyiwa tathimini ya gharama za nyumba zao .

Kapufi amefafanua  kuwa  wananchi hao baada ya kuwa wamewekewa wameshindwa  kuendeleza  majengo mengine ya nyumba  na wao  wametii maelekezo hayo  kwanini sasa wao wanao washindwe kulipwa fidia zao .

Meneja  wa Taroads Mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende ameeleza kuwa swala la wananchi hao tayari lipo kwenye ngazi ya Wizara huku Mkoani wao wameisha tekeleza yale waliopaswa kufanya .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko amesema kuwa swala la wananchi hao juu ya madai yao ya fidia  Serikali inalitambua na wanafahamu wanaichi hao wana dai fidia kwa ajiri ya kupisha ujenzi wa barabara za kiwango cha lami.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages