Muonekano wa Nyumba ya Khadija Eneriko iliyopo Mtaa wa Shanwe ambayo imebomoka na kusabisha kifo cha Elizabeth Fabiano usiku walipokuwa wamelala |
Na Paul Mthias -Katavi.
Mkazi mmoja wa Mtaa wa Shanwe Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi amefariki dunia baada ya kuangukiwa na nyumba usiku alipokuwa amelala.
Mkazi mmoja wa Mtaa wa Shanwe Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi amefariki dunia baada ya kuangukiwa na nyumba usiku alipokuwa amelala.Khadija Eneriko Mkazi wa Mtaa wa Shanwe aliyepoteza Mtoto wake kwa kuangukiwa na nyumba
Akizungumzia
tukio hilo mama mzazi wa Marehemu Khadija Eneliko amesema mtoto wake Elizabeth
Fabiano amekutwa na madhila ya kifo hicho usiku wa kuamkia Jumapili ya
16/4/2023 walipokuwa wamelala kwenye nyumba hiyo.
,,tulipokuwa
tumelala kidogo usiku tukasikia Mvua inanyesha na baada ya muda kidogo
tukasikia ukuta wa nyumba unaanguka kwa nguvu na hapo mwanangu ukuta
ukamdondokea sehemu ya Mgongo na maeneo mengine ya mwili ‘’amesema Khadija
Ameeleza
kuwa baada ya hapo aliomba msaada kwa majirani na walimpeleka hospital lakini
akiwa anapatiwa matibabu alifariki Dunia
Rehema
juma mkazi wa Mtaa wa shanwe amesema kuwa Marehemu alikuwa anaishi na jamii
katika mwenendo uliomwema na wamesikitika kwa janga hilo ambalo limepelekea
kupoteza uhai wake.
‘’Tunaomba
serikali iweze kuangalia uwezekano wa kumjengea nyumba nyingine Bibi huyu kwani
hapa alipo mazingira siyo salama nyumba bado inaonekana kuwa na mipasuko
mipasuko lolote la weza kutokea ,,
Waombolezaji wakiwa katika Msiba wa Elizabeth Fabiano alefariki kwa kuangukiwa na Nyumba Mtaa wa Shanwe. |
‘’Ukiangalia
huyu Bibi ni Mjane na umri wake umeenda ila siamini kama yupo katika Mfuko wa
Tasaf angeunganishwa huko labda angeweza hata kukalabati nyumba yake amesema
Msafiri ,,
Mjumbe
wa serikali ya Mtaa wa Shanwe lazaro Saimon Kakamba amesema tukio hilo
limetokea kwenye mtaa wake na wamesikitishwa na tukio hilo.
Kakamba
ameiomba serikali kuangalia uwezekano wazee wasiojiweza kuingizwa katika mfuko
wa Tasaf ili waweze kuendesha maisha yao.
‘’Viongozi
wanakuja hapa mara tupo kufanya tathimini kila siku tunadangaywa labda 2030
hiyo Tasaf tutaipata’’ amesema Kakamba.
Nyumba hiyo imejegwa zaidi ya miaka 45 iliyopita wakati Khadija Eneliko akiwa na Mme wake.