Na Walter Mguluchuma -Katavi
Idadi ya watu wanaojitokeza kupata chanjo kwenye vituo mbalimbali vinanyotolea huduma za Chanjo imeongezeka kutokana na hamasa kubwa inayotolewa na na Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali ikiwepo taaasisi ya TAYOBECO na kufanya watu waone umuhimu wa chanjo ya UVIKO 19 na chanjo za aina nyingine .
Moja ya washiriki wa kikao hicho akitoa maoni yake juu ya mradi huo |
Amesema kuwa idadi ya
watu wanaojitokeza kwenye vituo vya
kutolea chanjo ya Uviko 19 imeongezeka
kufatia wananchi kupata uwelewa
kutokana na mradi wa Boresha Habar toka i ulipoanza kufanya kazi kwenye
Manispaa ya Mpanda kwa kushirikiana na Serikali .
Kumburu amefafanua kuwa vyombo vya habari vimesaidia pia kuwafanya wananchi watambue umuhimu wa wa huduma ya chanjo ya UVIKO 19
lakini pia hata magonjwa mengine ya mlipuko wa
janga la surua lililokuwa limeukumba Mkoa wa Katavi .
Hivyo hata
watowa huduma za afya kwa jamii(CHW) hawakuangaika sana kuwafikia
wananchi na kuweza kupata uwelewa moja kwa moja juu ya
umuhimu wa hizi huduma za chanjo mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa
kwenye vituo vya kutolea chanjo .
Ametowa
mfano wa chanjo ya UVIKO 19 hapo awali
vituo ambavyo vilikuwa vituo taarifa vilikuwa havifiki kumi vituo vingine vilikuwa vina sua sua watu walikuwa na dhana potofu juu ya huduma
hizi za chanjo lakini kutokana na mradi
wa TAYOBECO umesaidia sana kuongeza
nguvu ya uwelewa kwenye jamii na ndio maana leo wanavituo 28
ambavyo vinalipoti huduma za UVIKO 19 .
Lakini
pia vinaripoti magonjwa mengine ukiwepo ugonjwa wa mlipuko wa
surua hii yote imetokana na mchango mkubwa ambao TAYOBECO wamewekeza hususani kwa watowa huduma za afyana
ndio chanzo cha hayo mafanikio yote
mpaka leo wanafikia idadi kubwa
ya mwitikio wa watu kupata chanjo
na pindi wanapokuwa wameona kuwa na dalili za kupata magonjwa ya mlipuko
moja kwa moja wanakwenda kwenye vituo vya kupatia chanjo .
Program Meneja
wa shirika la Tanzania Youths Behevioral
Organization(TAYOBECO)Adinani Mussa amesema kuwa kwa zaidi ya miaka mitatu sasa shirika la INTERNEWS Tanzania limekuwa
likitekeleza mradi wa boresha
habari unao fadhiliwa na USAID
Lengo
la mradi huu ni kuwahamasisha vijana
na wanawake umuhimu wa chanjo ya Uviko
19 pamoja na chanjo nyingine mbalimbali ikiwemo chanjo ya surua na kwa makundi mengine mbalimbali wakiwepo na
wazee .
Adinani
Mussa amebainisha kuwa kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa hivi karibuni Mkoa wa
Katavi ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa na mwitikio mdogo wa chanjo ya
uviko 19 na ndio maana wakaona mradi huu wa Boresha habari kuuleta katika Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi .
Mtoa
huduma za afya ngazi ya Jamii katika Kaya ya Mpanda Hotel kwenye kituo cha Afya
Mwangaza Jolald Makori amesema toka mradi huu ulipoanza mwanzoni mwa mwezi wa Februali
ameweza kuhamasisha watu 441 ambao wameweza kuchanja chanjo ya Uviko 19 ambapo
hapo awali kwenye kituo hicho walikuwa hawazidi watu mia moja .
Ameeleza kuwa mradi huu watu wameupokea vizuri na watu
wamehasika kuchanja na wala
hawakuangaika sana kwa kuwa watu
walikuwa wamehamasika kutoka na elimu iliyotolewa na mradi wa Boresha Habari .