Shekhe mkuu wa Mkoa wa Katavi Mashaka Nassoro Kakulukulu akitoa neno la shukurani kwenye futari iliyoandaliwa na Eng Isamail Ismail nyumbani kwake eneo la Nsemlwa kwalakwacha |
Jamii katika mkoa wa Katavi imeaswa kuishi kwa upendo na Amani bila kujali itikadi zao ili kuwa na jamii inayomchamungu.
Jamii katika mkoa wa Katavi imeaswa kuishi kwa upendo na Amani bila kujali itikadi zao ili kuwa na jamii inayomchamungu
Wito
huo umetolewa na shekhe mkuu wa mkoa wa katavi Mashaka nassoro Kakulukulu
wakati akitoa neon la shukurani kwenye Futari Iliyoandaliwa na Eng Ismail
Ismail nyumbani kwake Eneo la Kwalakwacha Manispaa ya Mpanda.
Kakulukulu
amesema kuwa hiki kinachofanyika cha kujumuika kwa pamoja bila kujali itikakadi
wala Imani ya mtu ni ishara upendo na mshikamano kwenye jamii ya wanakatavi.
‘’kitendo
hiki kilichofanywa na Ndugu Ismail ni kuonyesha kuwa sisi wanajamii yatupasa
kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kijamii bila kujali huyu Mwislamu au
Mchristo kwa vile Imani zetu zote zinasisitiza umoja Amani na mshikamano’’
amesema Shekhe Mashaka.
Khadija
kipingu mkazi wa Kichangani alieshiriki katika Futari hiyo amesema anaishukuru
familia ya Eng Ismail kwa kuonyesha upendo kwa jamii kwa kuandaa futari hiyo
kwa jamii ikiwa ni sehemu ya kumucha mungu kwa kuonyesha upendo bila kujali
Imani ya Mtu.
‘’Hii
inaashiiria umoja na mshikamano tumeweza kushiriki kwenye Futari hii watu wa
itikadi tofauti,Amani na umoja ndio msingi wa maendeleo ya wanajamii ‘’amesema
Lupamba
Kwa
upande wake Eng Ismail Ismail amesema amemua kufanya tendo hilo la kufutulisha
ikiwa ni ishara ya upendo inayoambatana na kupata Baraka kutoka kwa mwenyezi
mungu kwa kutoa sadaka kama quran inavyo elekeza.
‘’Ninawashukuru
wananchi wote waliofika katika hafla hii ya futari niliyoiandaa hapa leo
tumejumuika kwa pamoja nimefurahi kuona jamii yangu inajumuika kwa pamoja na
mimi kwenye shuguli hii’’amesema Ismail.
Mhandisi Ismail Ismail amesema anaishukuru jamii kwa kumuunga mkono kwa kushiriki katika futari aliyoiandaa. |
Futari
hiyo imehudhuliwa na Viongozi wa Serikali,Viongozi wa Vyama vya siasa Taasisi
na watu Binafsi.